KUMJUA MUNGU

Share it Please

 





KUMJUA MUNGU NI CHANZO CHA MAFANIKIO YAKO YOTE
21 Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia.
Ayubu 22:21

Kumjua Mungu ni kuwa na ufahamu wakutosha kumuhusu Mungu.Unafamu yeye ni nani ,ana nguvu kiasi gani, uweza alonao nk hii inatufanya tujiweke chini ya utawala wake Na kutoa Maisha yetu yote kwa kwake .

Kufanikiwa kibiblia ni kuwa vizuri maeneo yote kwenye maisha Na wanadamu wengi tunapenda kufanikiwa, kila mmoja yupo busy eneo Lake kuhakikisha anafanikiwa ila kutokana na andiko hapo juu tunapaswa kumjua Mungu sana sio kidogo na mafanikio yatakuja tu sio kuyatafuta.
Ni vizuri kujua kuwa Mungu ametuandalia kila tunachohitaji kwenye maisha yetu na kinapatikana kwaajili yetu ila tunavielewa na kuvipata kwa kumjua Mungu.
3 Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.
2 Petro 1:3

Uweza wa uungu umetukirimia (Umetupatia) kila tunachohitaji kwaajili ya uzima(maisha yetu ya mwilini) na utauwa(maisha yetu ya Rohoni) kwa kumjua yeye. Hii inamaana hivi vitu hatuwezi kuvipata kama hatamjua yeye aliyetuita kwaajili ya utukufu wake mwenyewe.

Weka shauku, matamanio yako kumjua sana huyu Mungu mwenye vitu vyako vyote unavyovihitaji. Usiweke jitihada kutafuta vitu weka jitihada ya kumtafuta Mungu mwenye vitu.
#ZaidizaidinikufahamuYesunijuependolakonawokovuwakokamili

Na mchungaji Imani Boaz



No comments:

Post a Comment