Showing posts with label Mahusiano. Show all posts
Showing posts with label Mahusiano. Show all posts

BINTI WA TB JOSHUA AFUNGA NDOA KATOLIKI NA MTANZANIA

 

 


 

Na Mwandishi Wetu,

Jiji la Arusha jana lilikuwa na hekaheka kubwa ya kushuhudia ndoa ya mtoto wa Nabii wa Nigeria, Temitope Balogun Joshua maarufu kama TB Joshua, Serah Joshua iliyofanyika katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Moyo safi wa Bikira Maria iliyopo Unga Limited.

Ndoa hiyo ya Serah Joshua kwa Mtanzania Brian Moshi ilifungwa na Paroko wa Kanisa hilo, Festus Mangwangi .

Binti huyo ni miongoni mwa watoto watatu wa T B. Joshua aliyezaliwa Juni 12, 1963.

TB Joshua ni mmoja ya manabii maarufu na mwasisi wa kanisa la The Synagogue, Church of All Nations (SCOAN), kanisa linaloendesha pia televisheni ya Emmanuel yenye matangazo ya kikristo kutoka Lagos , Nigeria.

Akihubiri wakati wa kufungisha ndoa hiyo, Paroko Mangwaji alisema kufungwa kwa ndoa hiyo kumeiunganisha nchi ya Tanzania na Nigeria.

Alisema ndoa hiyo ni ushuhuda wa malengo ya Hayati Baba wa Taifa Julius Nyerere ya kutaka Bara la Afrika liwe kitu kimoja na kuwa sasa yametimia baada ya ndoa hiyo.

Padre Mangwaji alisema yapo mengi yanayounganisha watu ikiwa ni pamoja na masomo na kuoana na kuwa yanapotokea mambo hayo huondoa uwezekano wa kubaguana.

“Serah huko Nigeria umeona wanaume wengi lakini umempenda Brian na Brian hapa Sinoni au Marekani uliona wengi lakini umemchagua Serah, wanangu nawaombea mkazae matunda mema kwa sifa na Utukufu wa Mungu,” alisema.

Alisema ndoa hiyo ya mume na mke mmoja kwa taratibu za Kanisa Katoliki, ilitangazwa kanisani hapo mara tatu kuanzia Aprili 11,2021 hadi Mei 2,2021 na hakukuwa na pingamizi lolote na kuamua ifungwe.

Padre Mangwaji aliwataka maharusi hao kuzaa watoto nane ili Kanisa lipate watawa na kuja kuwasaidia katika kazi ya kuhuburi neno la Mungu.

Ndoa hiyo ilihudhuriwa na wageni kutoka Lagos, Nigeria na Marekani, wanaposoma Brian na Serah.

Mke wa Tb Joshua na mama wa Serah, Evelyn Joshua alisema hii ni mara ya kwanza kuja nchini Tanzania na amekuja kushuhudia ndoa ya mtoto wake.

Alitumia pia alitumia nafasi ya harusi hiyo kushukuru muungano huo na kuongeza kuwa anacho cha kusimulia akirudi nchini Nigeria.

Desemba, 2020, Nabii TB Joshua alishindwa kuhudhuria harusi ya binti yake nchini humo kutokana na maagizo yanayolingana na waji bu wake.

Kwa mujibu wa mtandao wa Opera News TB Joshua alikuwa anapokea maagizo kwa ajili ya mwaka 2021.

Aidha alisema kwamba kuna umuhimu wa kusikiliza maneno ya Mungu hata ni magumu sana kwako.

Chanzo: Habari Leo

Read More

Wanaume kabla ya kuoa huangalia mwanamke mwenye sifa hizi

 

 

 

 

Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi kuchunguza mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa pamoja kwa kipindi chote cha maisha.

Wanawake wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachoweza kuwafanya wakapata wachumba ni uzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na kujiremba ili wawavutie wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya uzuri.

Hali sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na sura nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa.

Utafiti ambao nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzuri wa tabia na umbo, kuna kuna sifa nyingine za msingi ambazo mwanamke anatakiwa kuwa nazo ili aweze kuwa katika mazingira mazuri ya kupata mchumba wa kumuoa kiasi kwamba asipokuwa nazo ataishia kuchezewa tu lakini haitatokea mtu kumtakiwa kwamba anataka kumuoa.

1. Mwenye mapenzi ya kweli.

Lengo kubwa la mwanaume kuoa ni kutaka kupata mapenzi ya kweli kutoka kwa mwanamke na ikiwezekana waweze kupata watotoa ambapo watoto hao ndio furaha ya ndoa. Wapo wanawake wengine ambao wanonesha wazi kutokuwa na mapenzi ya kweli bali wanakuwa na mapenzi ya kuzuga. Wanachotaka wao aidha kupata umaarufu tu kwamba yuko na mtu fulani ama kuweza kupata pesa alizonazo mwanaume lakini sio kwamba ana mapenzi ya dhati kutoka moyoni mwake.

Mwanamke asiye na mapenzi ya dhati utamgundua tu, muda mwingiutamuona macho yake yako kwenye mfuko wa mwanaume. Akiona kwamba mfuko umetuna utaona anaonesha mapenzi ya hali ya juu lakini pindi hali inapokuwa kubwa mbaya kifedha mapenzi yanaanza kufifia.

Kwanini wanaume wanapenda wana wake wenye mapenzi ya dhati kutoka mioyoni mwao na si kutokana na fedha walizonazo? Hii inatokana na ukweli kwamba maisha siku zote yanabadilika, kama waswahili wanavyosema, kuna kupanda na kushuka.

Sio kwamba kila siku utakuwa na maisha mazuri na kama itatokea hivyo basi ushukuru mungu.Hivyo basi mwanamke wa kuoa lazima afahamu hivyo na awe tayari kuonesha mapenzi yake ya dhati wakati wote wa maisha yao na si kwa kipindi fulani tu cha neema.

Si hivyo tu pia asilimia kubwa ya maisha ya ndoa yanatawaliwa na mapenzi, kwa hiyo nyanja hiyo inakuwa ya msingi sana kwa wanaume wengi kuiangalia ili wasije wakajikuta wanaoa mwanamke ambaye baada ya muda mapenzi yanakwenda likizo hali ambayo inaweza kuwafanya wasiishi maisha ya raha mustarehe.

2. Wenye tabia nzuri

Tabia njema ndio silaha ya maisha, ukiwa na tabia nzuri kila mtu atakupenda, hiyo ni katika maisha ya kawaida. Lakini linapokuja sualana kuoa tabia inakuwa kitu cha awali sana kungaliwa na hiyo inaweza kuwa na ukweli kwa sababu wapo wasichana wazuri wenye mvuto wa aina yake na maumbile mazuri, lakini wanakosa wanaume wa kuwaoa, ukiuliza kwani utaambiwa anatabia mbaya.

Naweza kusema hilo ndilo limekuwa tatizo kubwa kwa baadhi ya wanawake kukosa wanaume wa kuwaona. Hakuna mwanaume hata mmoja kati ya wale ambao nimejaribu kuongea naye ambaye ameonesha kulidharau suala hilo la tabia.

Si hivyo tu wapo wanaume ambao wameingia kichwa kichwa na kuoa kwa kuangalia sura tu bila kujali tabia, matokeo yake baada ya siku chache yanatokea machafuko ya aina yake hali ambayo imepelekea kuvunjika kwa ndoa kutokana na tabia mbaya alizonazo mwanamke.

3. Mwenye uchu wa maendeleo

Hivi karibuni kumekuwepo na mabadiliko ya aina yake kwa wanaume, wengi sasa hivi hawapendi kabisa kuoa mwanamke ambaye hana kazi yaani ‘golikipa’. Kama atakuwa hana kazi basi awe na uchu wa maendeleo kwa kujituma kufanya kazi mbalimbali za kimaendeleo kama vile kilimo kwa wale walio vijijini na biashara ndogondogo kwa wale ambao wako mijijini na hata vijijini.

Ile dhana ya kusema mwanamke ni mama wa nyumbani wa kukaa na kujipodoa akimsubiria mwnaume arudi amstarehesha, sasa hivi imepitwa na wakati. Wanaume wengi wanapenda wanawake ambao ni wahangaikaji, wenye ndoto za maendeleo katika maisha yao. Hata kama watakuwa si wafanyakazi lakini wawe wenye kutoa ushauri kwa waume zao juu ya jinsi gani wafanye ili wafanikiwe.

4. Wasiopenda makuu.

Kuna wanawake wengine wanakuwa na tabia za ajabu sana kiasi kwamba yaweza kuwa kero kwa wanaume. Wapo wanawake ambao wanapenda makuu bila kujali hali halisi ilivyo. Kuna wanawake naweza kusema wana tamaa, kila wikiendi utamsikia “leo tunakwenda wapi dear?”

Akimuona rafiki yake kanunua simuya laki tatu na yeye utamsikia akisema, ‘na mimi naomba uninunulie simu kama ya Grace’. Ukienda naye Pub anakuambia,”mimi sinywi pombe za chupa natumia za kopo tena Heineken’. Yeye hajali kiasi cha pesa mwanaume alicho nacho na usipotekelezea anachukia na anaweza hata kupunguza mapenzi.

Wanawake kama hawa wako katika mazingira magumu sana ya kuweza kupata wanaume wa kuwaoa. Mara nyingi katika maisha fedha huzungumza, kama mwanaume atakuwa na pesa ya kutosha itakuwa rahisi sana kwa mwanamke kupata kila atakachopenda lakini si kwa kumwambia mimi nataka kitu fulani.Mwanaune mwenyewe utamsikia akisema, ‘unataka nikununulie simu ya aina gani, au leo unataka twende wapi?’ hapo ndipo utakuwa na nafasi ya kusema, ‘mimi nataka uninunulie simu kama ya fulani ama leo nataka twende sehemu fulani.’

Wanaume ni warahisi sana wa kuwapatia wale ambao wanatarajia kuwaoa chochote ambacho watahitaji kama tu pesa haitakuwa tatizo. Kitu ambacho kinawaudhi wanaume wengi ni ile tabia ya mwanamke kupenda mambo makubwa bila kuangalia uwezo uliopo kwa mwanume.

Kuna wanawake wengine wao si wasemaji kabisa, yeye anasubiri leoamemletea hiki, anapokea na kushukuru, kesho akiambiwa twende beach anakubali. Au wengine wanasubiri mpaka waulizwe wanataka nini, ndio wanasema.

Sisemi kwamba uwe mkimya tu hata kama una shida ya kitu fulani na unafahamu kwamba ukimweleza mwenza wako anaweza kukusaidia, hapana! kama unaona kwamba uwezekano wa kupata kile ambacho unakihitajiupo mweleze kwa utaratibu naamini atakuelewa na kukutimizia.Tabia ambayo hawaipendi wanaume wengi ni ile ya kulazimisha ufanyiwe kitu fulaniwakati inawezekana uwezekano haupo.

5. Wavumilivu.

Wapo wanawake ambao sio wavumilivu kabisa katika maisha.Tunajua kwamba maisha siku zote hayatabiriki, yanaweza kutokea matatizo ya kiafya ama kifedha.Huu ndio wakati wa kuona uvumilivu wa mtu.Kama mwanamke anatarajia kwamba siku zote ni za raha tu na pindi matatizo yanapotokea anachukua uamuzi wa kumtoroka mwanume, huyo siyo mwanamke wa kuoa.

Wangapi leo hii huwatoroka waume zao pindi inapotokea kuumwa, kufilisika ama kupatwa na tatizo lolote ambalo kwa namna moja ama nyingine yanaweza kuwafanya maisha yao kutingishika?

Uvumilivu kwa mwanamke utakuwepo kama tu atakuwa na mapenzi ya dhati kama nilivyozungumza hapo awali. Mwanamke mweye mapenzi ya dhati ni lazima atakuwa mvumilivu na atakuwa tayari kuishi katika maisha ya aina yoyote, yawe ya raha ama ya starehe.Hawa ndio wale ambao wanaume wengi wengependa kuwa nao maishani mwao.

Kwa maana hiyo basi hiyo iwe changamoto kwa wanawake. Wajue kwamba wanaume wanafurahi kuwa na wanawake wa aina gani. Hata kama utakuwa umeshaolewa, kama kuna wakati kunakuwa na kutokuelewana baina yenu, chunguza yawezekana kwamba unakosa mojawapo ya tabia ambazo nimezitaja hapo juu. Waweza kubadilika kwani inawezekana.

 

SOURCE MUUNGWANA BLOG 

Read More

Vyakula vya Kuepuka Kula kwa Wanaume

 

 Katika makala hii hii utajifunza vyakula mbalimbali ambavyo wanaume hawatakiwi kula ili kubaki na afya bora wakati wote. Kuna vingine unaweza kuwa unavitumia kila siku bila mwenyewe kujuwa.

Punguza kula vyakula feki kuzuia kupoteza nywele

Moja ya matatizo makubwa upande wa urembo kwa wanaume ni kupoteza nywele (upala). Lakini kama unatafuta kitu cha kukilaumu dhidi ya tatizo lako la kunyonyoka nywele basi ni hiyo sahani yako ya chipsi unayokula kila siku.  Vyakula feki (junk foods) ni hivyo vinapatikana kwenye fast foods na takeaway centers nyingi hasa mijini kadharika vyakula vile vyote vya kwenye maboksi.

Vyakula hivi feki vina kiasi kingi mno cha lehemu (cholesterol) na lehemu hii hupelekea kile huitwa kwa kitaalamu kama ‘pregnenolone’ na kupelekea kiasi kikubwa cha ‘dihydrotestosterone’ (DHT) na hatimaye kupotea kwa nywele kichwani a.k.a upara.
Kunyonyoka kwa nywele kunaweza kuwa ni jambo la kurithi (genetics) lakini vile vile aina ya chakula unachokula kinaweza kuwa kinahusika moja kwa moja.

Punguza kunywa pombe 
Wanaume wengi wanaokunywa bia kupita kiasi huwa na uwezekano mkubwa wa kupatwa na tatizo la kuota matiti kama wamama tatizo lijulikanalo kwa kitaalamu kama ‘gynecomastia’.

Kwenye bia au pombe mara nyingi hakuna lishe ya moja kwa moja na hivyo hukufanya ujisikie njaa au hata kuongzeka kwa njaa zaidi na ndiyo sababu unaambiwa kama huna uhakika utakula wapi ni bora usinywe pombe ili kulinda afya yako.

Kwenye bia kuna kitu kama homoni ya oestrogen ya kupandikizwa na hivyo unywaji pombe kupita kiasi kuna uhusiano wa moja kwa moja na matokeo ya wanaume kuwa na matiti kama wanawake.

Acha kutumia mafuta ya mboga mboga kuepuka saratani ya tezi dume
Mafuta yatokanayo na mboga mboga au mimea yamekuwa yakipigiwa debe kwa miaka mingi na watu wanaojihusisha na lishe na wale wenye hasira sana na mafuta yatokanayo na wanyama. Hata hivyo leo nakujulisha mafuta hayo si salama sana kutumika na mwanaume kila siku. Hili limekuja hasa kutokana na kuongezeka kwa magonjwa ya moyo na lehemu na watu walazishwawa kutumia mafuta ya namna hiyo.

Lakini mafuta haya ya mboga mboga ndiyo kitu kibovu kabisa unatakiwa kukiepuka ili usipatwe na saratani ya tezi dume.  Linapokuja suala la kujilinda saratani ya tezi dume basi mafuta yenye omega 3 ndiyo suluhisho la kudumu na siyo omega 6 kama ilivyo kwenye vyakula vingi vya kwenye makopo, mafuta ya alizeti, maharage ya soya, mafuta ya  canola na mafuta ya corn na mengine yote yenye omega 6.

Popcorn
Popcorn au bisi ni chakula kingine mwanaume hatakiwi kula, hupikwa kwa kutumia mafuta yasiyo na afya, sodiamu nyingi na ni chanzo cha baadhi ya kansa. Kuna kitu kinaitwa ‘Diacetyl’ kinachopatikana kwenye popcorn ambacho kinahusika na kusababisha kansa na kuna kingine kiitwacho ‘Perfluorochemicals’ ambacho huathiri tezi ya thyroid na ugonjwa wakati huo huo husababisha ugonjwa wa kupungukiwa umakini ujulikanao kwa kiingereza kama ‘Attention-deficit/hyperactivity disorder (ADHD)‘.Ni vizuri kuacha kula popcorn.

Mkate mweupe
Mkate mweupe una wanga mwingi zaidi usio na faida. Kwenye hatua za kutengeneza mkate mweupe vitamini zote za kundi B hupotea, hupotea pia nyuzinyuzi (fiber). Siyo hivyo tu mkate mweupe umesemekana kuwa ni sababu ya ugonjwa wa kisukari na kuongeza uzito zaidi mwilini wakati huo huo ukisababisha tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu sana.

Vingine vinavyofanana na na hilo ni ugali wa sembe, tambi nyeupe, chai ya rangi na kahawa. Kula mkate ambao ngano yake haikukobolewa (brown bread), kula ugali wa dona na chai unaweza kutumia tangawizi au mdalasini badala ya majani ya chai.

Chumvi ya mezani
Chumvi ya mezani ile ya unga nyeupe haifai kwa mwanaume. Kila mmoja amesikia chumvi hii husababisha shinikizo la juu la damu na pamoja na hayo bado sehemu kubwa ya watu wanatumia chumvi hii.

Chumvi ya mezani husafishwa kwa kuondoa madini, madini na hupitishwa katika joto la nyuzi joto. Kwa hiyo uliyonayo sasa ni asilimia 40 ya sodiamu na asilimia 60 ya kloridi, na kisha kemikali kama vile ‘aluminium silicate’ huongezwa ili kuifanya isishikane na hivyo kubaki katika hali ya unga. Aluminium silicate ni sumu kali inayoharibu mfumo wetu wa fahamu. Inatajwa kuwa ni miongoni mwa sababu zinazosababisha ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu (Alzheimer).

Chumvi ya mawe ya baharini ile ambayo haijapita kiwandani (unrefined sea salt) ndiyo nzuri zaidi kwa afya ya mwanaume.

SOURCE, MUUNGWANA BLOG, 27/3/2021

 

Read More

Maneno ambayo unapaswa kumwambia mpenzi wako ili kuongeza ladha katika mahusiano


 Mapenzi yanayotawaliwa na maneno matamu hunawiri na kuchanua kama mmea uliopandwa kando ya mto. Hakika maneno mazuri husadifu mambo mengi mazuri baina yenu ikiwemo upendo, kujali, kuthamini, heshima, utii, upole, nidhamu, uaminifu, unyenyekevu, usikivu, ukarimu na faraja hivyo ni vema kuhakikisha kama kweli unampenda kinywa chako daima kimtolee lugha nzuri ya maneno matamu.


Weka desturi ya kusema mambo haya kwa mwenza wako hakika inazidisha furaha na amani kati yenu..

Nakupenda

Nakupenda ni kitu rahisi na cha wazi cha kumwambia mwenza wako. Hakikisha tu kuwa unamaanisha. Jaribu kulisema neno hilo pindi mwenza wako anapokuchekesha au pale anapofanya kitu kinachokukumbusha kwanini mko pamoja.....```

Umependeza
Kama umekuwa kwenye ndoa kwa muda mrefu, ni rahisi kujisahau katika mengi. Ni muhimu kumkumbusha mwenza wako kuwa anakuvutia. Kumjulisha kuwa ulivo vaa umependeza sana’ kutamfanya ajisikie vizuri na kukumbusha kwanini ulimchagua yeye.

Samahani
Kila mtu hukosea wakati fulani. Wakati mwingine hujikuta tukiongea maneno kwa hasira na baadaye kugundua kuwa hatukuwa sahihi. Ubishi hauna nafasi kwenye ndoa ya wenye furaha, hivyo omba msamaha unapofanya kosa. Omba msamaha kwa kukasirika. Omba msamaha kwa kuumiza hisia za mwenza wako..```

Nilikuwa nakuwaza
Ni muhimu kumjulisha mwenza wako kuwa unamuwaza hata kama hamko sehemu moja. Ukiona kitu kizuri au cha kuchekesha katika siku yako ambacho kinakufanya umkumbuke, mjulishe...```

Siku yako ilikuaje?

Muulize masuala ambayo mwenza wako anakutana nayo katika shughuli zake kazi kubwa waliyokuwa wakifanya. Kumpa nafasi mwenza wako kushare sehemu zingine za maisha yake kutasaidia kuumuweka sawa.```

Napenda mawazo yako.

Mwambie mwenza wako kuwa unapenda mawazo yake. Mjulishe kuwa unaona ana akili, mcheshi, anajua kupenda na ana kipaji.```

Nakuunga mkono

Mpe moyo mwenza wako kwa kumjulisha kuwa unaunga mkono maamuzi yake. Unaweza ukaenda mbali zaidi kwa kujaribu kumsaidia afanikishe malengo aliyojiwekea. Maisha yamejaa vikwazo vingi, na ile hisia kuwa una mtu mwingine upande wako zinaweza kukusaidia kuvivuka. Msiwe wanandoa tu, kuweni timu. Kumkumbusha mwenza wako kuwa upo nyuma yake kutaimarisha umoja wenu.

Hakuna kama wewe.
Mwenza wako anatakiwa kuwa rafiki yako. Kama hautaki kutembea naye, basi hamkupaswa kuwa pamoja. Mfanye mwenza wako ajue kuwa yeye ni bora na hakuna kama yeye.```
Read More

Jifunze kummsis mpenzi wako inasaidia sana

 


Jinsi ya kummisi mpenzi

Ni lazima uipe pumzi penzi lenu kama mnafanya kazi ambayo inawafanya wewe na mke wako kuwa pamoja kila wakati, basi kila mmoja anahitaji muda wa peke yake awe na muda wa kummiss mwenzake.


Huwezi kummiss mtu ambaye kila dakika unamuona, sana sana utaishia kuona mapungufu yake na kugombana tu. Utammiss vipi wakati kila wakati uko naye, kila mmoja anahitaji kummiss mwenza wake ili mapenzi yawe na raha.


Mume/mke wako anahitaji maisha mbali na wewe, anahitaji angalau nusu saa kwa siku ambayo hataona sura yako, atakuwa na watu wengine, atakuwa na marafiki au atakuwa anafanya kitu kingine bila wewe.

Kama uko kwenye ndoa au mahusiano ambayo kila kitu mnafanya pamoja, kila wakati mko pamoja, kila muda wa ziada mko pamoja basi suala la kugombana kwenu ni la muda tu.

Jifunze kuwa na furaha nje ya mwenza wako, si kuchepuka hapana, hata kucheza tu karata na majirani inatosha kukufanya ummiss mwenza wako.

Kama kila wakati mko pamoja, hata kama hamfanyi kazi pamoja lakini kama ule muda wa zaida kila siku mpo pamoja basi mtaanza kuboana, utaanza kuona mapungufu ya mwenza wako, utaanza kuona ubaya wake na mtagombana tu.

Yes kuna watu wanalalamika kuwa waume zao wanawaganda hawatoki nyumbani, kuna wanaume hulalamika wake zao wanawaganda.

Kama mnagandana kama mapacha halisi jua tu mtaboana.

Read More

Msichana mwenye sifa hizi huwa hakiwii kuolewa

 





Kuolewa ni heshima kwa mwanamke. Heshima hiyo inaenda mbali zaidi hadi kuwagusa wazazi wa binti ambaye ataolewa. Wazazi wanatembea kifua mbele pindi binti yao anapoolewa, tena wanafurahia zaidi binti huyo anapoolewa akiwa angali bado hajazaa.

Wanamshukuru Mungu kwa binti yao kujitunza. Wanamshukuru binti kwa kuwapa heshima katika familia yao na ndiyo maana siku ya sherehe ya kuagwa (send off) wazazi wanafurahi sana kuagana na binti yao kwa heshima.

Hali hiyo huwa inaleta shauku kubwa kwa warembo wengi kutamani kuingia kwenye ndoa. Wengi wanaguswa na rekodi za wanawake wenzao ambao wamejitunza na hatimaye kuwaletea heshima wazazi wao.

Kinyume chake, wengi wamejikuta wakijilaumu kwa kushindwa kuleta heshima katika familia zao. Binti umri unaenda, anatamani kuingia kwenye ndoa lakini hapati wa kumuoa. Au mwingine inatokea, anatamani kuolewa lakini anaishia kupigwa mimba na kuachwa.

Badala ya kuleta heshima, analeta aibu katika familia yake kutokana na mila na desturi zetu kumtaka binti azae pale tu atakapokuwa ameolewa. Azae pale atakapokuwa kwa mumewe na si vinginevyo. Inapotokea bahati mbaya basi ni mara moja na si kuzaa na kuzaa watoto kibao.

Pamoja na kuwa ndoa ni mpango wa Mungu lakini hivi umeshawahi kujiuliza wanaolewa wanakuwa na sifa gani? Kwa nini wanaume wanavutiwa nao? Wanakuwa na kitu gani cha ziada ambacho wanawake wengine hawana? Leo nitakuambia!

Jamani, sifa ya kwanza ambayo mwanamke anapaswa kuwa nayo ni ile hulka ya kuwa mke. Wanaume wengi huwa wanapenda kuishi na mwanamke ambaye ana ile sifa ya kuwa mke. Ninaposema sifa ya kuwa mke naamisha mwanamke ambaye atakuwa tayari kumlea mume na hata watoto.

Mwanamke ambaye atakuwa msaada kwa mwanaume wake pindi atakapokuwa na changamoto mbalimbali ikiwemo za maisha pamoja na maradhi. Mwanamke ambaye atajua thamani ya mume, ambaye atajua nini maana ya heshima kwa mumewe.


Mwanamke ambaye atamudu misukosuko ya maisha ikiwemo kufilisika, kuachishwa kazi na mengine magumu yanayofanana na hayo. Mwanamke ataka-yevaa sifa ya kuwa mke kwa maana ya kumhudumia mumewe pindi atakaporudi amechoka kutoka kazini.

Wanaoolewa ni wale pia ambao wanajua kushuka pindi wanapoona kumetokea kutoelewana. Wanawake wale ambao wanajua kumtoa uchovu wa maisha mwanaume. Mwanamke ambaye hasababishi makelele ya mara kwa mara kwenye ngoma za masikio ya mwanaume.

Mwanamke ambaye hana gubu. Mwanamke atakayeelewa kwamba muunganiko wa ndoa una pande mbili hivyo kuwajali ndugu wa pande zote mbili, ndugu zake na ndugu wa upande wa mumewe. Mwanamke ambaye atakuwa na muonekano wa mke kwa maana ya mavazi na hata mazungumzo.

Wanaoolewa jamani wanakuwa na sifa ya uvumilivu. Wanakuwa na hofu ya Mungu. Mwanamke mwenye hofu ya Mungu, anamuomba yeye ampatie mwanaume mcha Mungu na kweli inatokea. Kuna siri kubwa sana katika kumuomba Mungu ambayo wengi wetu hatuijui lakini ni vyema kumtanguliza yeye katika kila jambo.

Ukiwa na sifa hizo, hata kama hautakuwa na muonekano wa kimisi au kuwa na shepu bomba kama wanavyosema vijana wa kisasa, utaolewa tu na hizo ndizo sifa za mwanamke anayetaka kuolewa!
Read More

Funzo kubwa kwa wanawake wote walio kwenye ndoa

 


Kumuamsha mdada wa kazi saa 11 alfajiri na kuwaacha binti zako wamelala Ni kumuandaa binti wa kazi kuwa mke Bora kuliko wanao. 

Eti kumtumikisha dada wa kazi apige deki, apike, afue nguo, aoshe vyombo wakati wanao wanaangalia TV. Ni kumuandaa mdada wa kazi  kuwa mwanamke anayewajibika kuliko wanao.


Kumuacha binti wa kazi aandae watoto kwenda shule, awaandalie uji mapema, awalishe, awasafishe wakati wanao wanacheza gemu kwenye simu au computer Ni kumuandaa binti wa kazi kuwa mama na mlezi bora kwa watoto kuliko wanao.

Na kwakuwa yote hayo unayafanya kwa masimango na manyanyaso unamfanya mdada wa kazi kuwa jasiri mwenye kuzikabiri changamoto za ndoa yake kuliko wanao.

Ukimaliza kwa kusema mwanao akiwa hajui hayo yote, ndoa ikiharibika mnazunguka kutafuta maombi kwa wachungaji kumbe ninyi mmeharibu ndoa za watoto wenu.

Msiwasumbue wachungaji bali wewe kama mzazi mfundishe mwanao kufanya kazi kama vile afanyavyo mdada wa kazi ili naye mwanae aje kuwa mke mwema hapo baadae.

Read More

Mambo unayopaswa kuyaepuka katika mahusiano yako ya Kimahusiano na Mke au Mume

 


Unapokuwa na mpenzi wako katika mahusiano, epuka sana kufanya vitu vya aina hii ambavyo vitasababisha mahusiano yenu kufa.


1. Kuanza kuchelewa kutoka kazini mara kwa mara

Sio kwamba kila mtu anapochelewa kutoka kazini basi anakuwa sio mwaminifu, lakini zaidi ya asilimia 75 (kutoka kwenye tafiti) ya ambao wamekuwa na mahusiano nje wamekuwa wakitoa visingizio vinavyohusiana na kazi, vikao, mikutano na safari za kikazi, yamkini wewe ni shahidi wa hili.

2. Mazingira tatanishi ya simu 
Gafla simu zinaanza kumiminika mpaka mida ya usiku. Yamkini pia alikuwa yuko huru hata simu yake inapolia waweza ichukua na kumpatia lakini gafla anakuwa na hofu kubwa na kuificha simu yake, nimeongea na wengine ambao wanakwenda na simu hadi bafuni isije ikasikika.

Wengine wanaondoa milio katika simu zao wakati haikuwa kawaida yao, kuwe siri (password) ngumu hadi mwenyewe anashindwa kuikumbuka, wako ambao simu zao zikipigwa hawawezi kupokea na kuongea kwa uhuru kama kawaida, ataondoka na kujitenga pembeni akijifanya anaongea kiuaminifu kabisa.

3. Harufu ambazo hujazizoea
 
Kwa kuwa wapendanao huwa wamezoeana, mara nyingi hata aina ya manukato mmoja anayotumia yanakuwa yanajulikana kwa mwenzake, Sasa hembu fikiri unamkuta mpenzi wako ametokea na ana harufu ya tofauti kabisa na uliyoizoea, umeisikia harufu hiyo akiwa amerudi toka kazini wakati asubuhi alipoondoka alikuwa na harufu ile uliyoizoea.

4.Tabia za kuanza kukufuatiliasana au hata kukuganda.
Wapo wanaotawapeleka wapenzi wao kila wanakotaka, nakutoruhusu mazingira ya wapenzi hawa wakike kuwa huru kufanya mambo yao wenyewe, wengine waliitafsiri hali hii kama penzi kubwa lakini baada ya muda unagundua kuwa ile ilikuwa ni ujanja wa kuficha uhalisi wake na kuzuia mazingira kwa mpenzi wake kugundua au kupewa taarifa ya tabia zake.

5. Kuzungumza sentensi za kutatanisha: 
Unaweza kukuta katika mapenzi yenu mpenzi wako anaanza kuwa na sentensi ngumu na zisizo kuwa na msingi kwa mfano anasema “kwa jinsi hii sidhani kama tutafika” “mi siamini kama mapenzi yanadumu” “yani ndio maana watu wanashindwa kukaa na mpenzi mmoja” na mara nyingine anaweza kukuuliza baadhi ya maswali moja kwa moja ili kukuona utajibuje. Sentensi hizi zina chanzo moyoni, kuwa macho.

6. Tabia za kuficha fedha: 
Hii utaiona ghafla mpenzi wake anaanza kuwa na siri kuhusu fedha zake au matumizi yake, na wala hapendi kuulizwa ulizwa kuhusu suala hilo. Tabia hii ikidhihirika katika mapenzi yenu usichelewe kuchunguza maana kwa kukaa kimya unaweza kujikuta umechelea mwana na maji ya moto.

Read More

Tuwe makini, ndoa si jambo la mchezo!!

 



Katika maisha ya mwanadamu, kuna mambo mawili yaliyo muhimu zaidi. La kwanza ni uamuzi wa kumfuataYesu na la pili ni uamuzi wa kuoa. Tafakari, kuoa si sawa na kununua shati. Ukilichoka na shati unaweza kununua nyingine lakini, huwezi kumwacha mke wako hata kama ukimchoka. Neno la Mungu linatuonya hatari ya kuoa mwanamke asiye mchaji wa Mungu; Twasoma: “Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika; kuliko na mwanamke mgomvi, mchokozi” (Mithali. 21:19). “Kutonatona daima siku ya mvua nyingi, na mwanamke mgomvi ni sawasawa; 16atakaye kumzuia huyo huuzuia upepo” (Mithali. 27:15-16). Zingatia: Pengine mtu atasema, “mchumba wangu ana imani tofauti, walakini tukioana nitamfundisha.”Lakini ikumbukwe mara nyingi, baada ya kufunga ndoa, watu hubadilika asitake kufundishwa tena.Tukumbuke mfalme Sulemani alikuwa na hekima kuliko wanadamu wote. Walakini, alipata hasara kubwa kwa sababu aliwapenda wanawake wageni wasio mcha Mungu na matokeo yake badala ya kuwafundisha imani yake, “yeye mwenyewe alinaswa na imani yao” (1Wafalme 11:1-4). Basi tujiulize, je sisi tunayo hekima kuliko Sulemani? Ni bora mtu amfundishe mchumba kabla hawajaoana na kuhakikisha kuwa ameamua kumfuata Bwana kwa moyo wake wote na si kwa sababu ya ndoa, ndipo atakapokuwa na amani na furaha katika ndoa yake. Tukumbuke faida moja wapo ya kuoa katika katisa ni kupata mke alifundishwa maadili na wanawake waliomtangulia; Twasoma: “Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wautakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema; ili wawatie – wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na uwapenda watoto wao; na kuwa wenye kiasi, kuwa safi,kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe, ili neno la Mungu lisitukanwe” (Tit. 2:3-5). Hivyo ni dhahiri kuna faida kwa mkristo kujipatia mke aliyefunzwa maadili ya ndani ya kanisa. Zingatia: Kuna baadhi ya watu wamevutwa sana na maumbile au mambo ya kimwili ya wachumba wao lakini Biblia inatukumbusha kuchunguza mioyo yao zaidi kuliko sura ya nje; Tasoma: “Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa” (Mithali. 31:30). “Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana” (Mithali 19:14). Je unazijua sifa za mke mwema? Mungu ameeleza peupe; Soma: (Mithali 31:10-31)


HATARI YA KUOANA NA ASIYE MCHAJI WA MUNGU


Kama tulivyojifunza hako juu hatari moja wapo ya kuoana na wasio wachaji wa Mungu ni kuishia kuvutwa na upotofu na kuanguka kiimani; Twasoma:”Kwa kuwa atamkengeusha mwanao mume asinifuate, ili wapate kuabudu miungu mingine; ndipo itakapowaka hasira ya Bwana juu yenu, naye atakuangamiza upesi” (Kumbukumbu 7:4). Na hayo ndiyo yaliyomapata Suleima kama tulikwisha kuoona; Soma tena: (1 Wafalme 11:1-4) Tukumbuke ikiwa tutaanguka katika uovu, mwisho wake utakuwa ni kutupwa katika hukumu (adhabu ya milele); Twasoma: “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uachafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui,ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayo fanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.” (Galatia 5:19-21) “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauwaji, na wazizi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili” (Ufunuo 21:8) “Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani hilo ziwa la moto. Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.” (Ufunuo 20:14- 15) Zingatia: Ndoa ni kifungo hivyo tukumbuke tunapoana hatuna ruhusa ya kuacha hata kama wenzi wetu ni wabaya vipi; Twasoma: “Lakini wale waliokwisha kuoana nawagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe; lakini ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe.” (1 Wakorintho 7:10-11) “Mwanamke hufungwa maadamu mumewe yu hai, lakini ikiwa mumwe amefariki, yu huru kuolewa na mtu ye yote amtakaye; katika Bwana tu.” (1 Wakorintho 7:39)


Hivyo ni dhahiri tunaaswa kuwa makini tunapo wachagua wenzi wetu, tukikumbuka ya kuwa kifungo cha

ndoa ni mpaka kifo


–Betty Kipala

Read More

Kwanini ndoa nyingi leo zimejaa migogoro?

 



Mchungaji Peter Mitimingi akiwa na mkewe Patience

Ndoa katika jamii za kikristo zilikusudiwa kudumu na kuwa mfano wa kuigwa na ndoa za watu wengine katika jamii. Lakini cha kushangaza ndoa nyingi leo za kikristo zinavunjika kwa kasi ya kushtusha. Hii inashtusha na kushangaza kwa sababu sisi kama wakristo tumeacha kutembea katika mpango kamili wa Mungu. Kwanini hali hii inatokea? Kuna sababu nyingi kwanini ndoa zinakuwa na migogoro isiyoisha na ningine kutawanyika. Kuna sababu ndogo ndogo na zingine ni kubwa na za msingi.

Zifuatazo ni baadhi ya Sababu Kwanini Ndoa nyingi siku za leo zimejaa Migogoro, Marumbano na Kuvunjika vunjika.

USIOE AU KUOLEWA KWASABABU YA KUMSAIDIA MTU FULANI AU KUMUONEA HURUMA

1. Kuoa au Kuolewa na Mtu kwasababu ya Kumuonea Huruma.

• Kuoa au kuolewa na mtu kwa sababu ya kumuonea huruma ni moja kati ya sababu zisizo sahihi. Na inaonekana kuwa ni sababu moja ya kijinga pia.

•Ndoa zianazo oana kwa misingi ya kumsaidia mtu au kumwonea mtu huruma huwa hazina maisha.

2. Huruma ya Kujiona kuwa ni wewe Ndio Unawajibika.

Kumhurumia mtu na kujiona kuwa una wajibu wa kumsaidia ni vizuri, lakini kuolewa naye kwa sababu hiyo ni wazi kuwa ni jambo lisilo la hekima kabisa.


3. Ndoa niyathamani Kuliko Huruma ya Mahusiano.

• Ndoa ni kitu cha thamani zaidi kuliko mahusiano ambayo yamejijenga katika huruma.

Chukulia kwamba kama mhusika ana masaa sita tu kuishi baada ya ndoa. Kwa hiyo utaishi katika ujinga huo kwa masaa sita tu maana kinyume na hapo utaishi maisha yako yote ukiwa unajihisi mjinga zaidi na mwenye huzuni.

• Hiyo itakuwa ni sabau ya kuvunjika kwa ndoa hiyo kwa sababu utaonekana mbaya zaidi ya kabla hujaingia.


4. Kuoa au Kuolewa kwajili ya Kumsaidia Mtu Anayeteseka.

•Usioe au kuolewa na mtu eti kwasababu unaamua kumsaidia kutokana na shida Fulani.

• Mfano kuna baadhi ya watu utakuta mwanaume anaamua kumuoa msichana fulani eti kwasababu kule anakoishi wanamnyanyasa na kumtesa so anaamua amsaidie amuoe ili aishi naye.

• Hii ni sawa na ile ya ujinga wa kufikiri kwamba utaoa au kuolewa na mtu kwa matumaini kwamba utambadilisha mtu baada ya kuolewa au kumuoa ili afanane na wewe, dini yako au tamaduni zako.

• Kumbuka kwamba, kuwa na jitihada za kukubaliana sio kubadilika, sababu suala ndoa halina haja ya kuweka mabadiliko kwa mtu yeyote.

• Ukitaka kumbadilisha mwenzi wako usisubiri kwenda kumbadilishia ndani fanya hayo mabadiliko kabla ya kuingia ndani.


–Mchungaji Peter Mitimingi

Read More

Faida za kuishi bila michepuko katika maisha

 


Kama wewe ni mtu ambaye huchepui, nakupongeza sana na hamna ambacho unakikosa kutoka kwa mweza wako. Watu wengi wanafikiri kuna amani au furaha ambayo wataipata wakichepuka, ukweli ni kwamba kila siku wanazidi kukimbizana na wanawake wapya na hawakipati wanachokipata. Baki njia kuu, hata kama kuna foleni utafika unakoenda kwa amani na bila magonjwa.

Zifuatazo ndizo faida za kubaki njia kuu.
 Utapata ammani moyoni
·Utaepukana na magonjwa
· Utakuwa na Furaha isiyo elezeka
·Utajimini zaidi
 Mke wako atakupenda zaidi (atajua umeacha kuchepuka hata usipomwambia)
· Utafurahia tendo la ndoa zaidi (Michepuko haina chochote cha zaidi ambacho
·mkeo au mumeo hana)Utasonga mbele kimaendeleo
·Utapata muda mwingi wa kuwa na familia yako
Read More

Makosa yanayofanywa na wanawake wengi katika mahusiano ya kimapenzi

 

Hakuna kitu kizuri kwenye uhusiano kama kuishi vizuri, uhusiano usiwe na ugomviugomvi wa kila mara. Kila mmoja aujue wajibu wake kwa mwenzake, amsome mwenzake ni mtu wa aina gani ili kuweza kujua namna ya kuishi naye. Mathalan ni vyema kumsoma mwenzi wako kama ni mtu wa hasira sana, ujue namna ya kuishi naye. Anapokuwa na hasira, usimueleze kosa lake au kumkosoa. Subiri hasira zitakaposhuka, mueleze katika lugha rafiki na hapo utakuwa umeepusha mengi.

Kumueleza mtu makosa yake katika wakati ambao naye ana hasira, utasababisha hasira zimpande zaidi na kusababisha hata ugomvi mkubwa hivyo busara zaidi zinapaswa kutumika. Mjue mwenzi wako ni mtu wa aina gani kisha ishi naye kwa staili unayoona inafaa. Kuna makosa mengi ambayo huwa wapendanao wanayafanya lakini katika makala haya leo nitazungumzia makosa ambayo ni hatari na yanafanywa na wanawake kwa wanaume wao.

Kung’ang’ania jambo
Mara nyingi wanaume huwa hawapendi kuona mwanamke anang’ang’ania jambo moja kwa muda mrefu. Hawapendi kuona mwanamke anashinikiza jambo kwa kiasi ambacho kinamnyima amani. Hata kama unajua upo sahihi, mwanamke unapaswa kutoonesha uking’ang’anizi kwa mwanaume wako. Mueleze mara moja jambo, mara ya pili ukiona hakuelewi muache kwanza.

Anakuwa anapima jambo lako na wakati mwingine akili yake inakubaliana na kile unachomueleza lakini namna unavyomng’ang’ania, unavyomshinikiza anaweza akajisikia vibaya. Mueleze mara moja, mara ya pili kisha wewe hamia kwenye mada nyingine. Utamkumbushia tena kesho au kesho kutwa na si lazima utake jambo hilo umueleze siku hiyo na siku hiyohiyo upate jibu la kueleweka. Anaweza asikuelewe siku hiyo lakini kesho yake ukaona mwenyewe ametekeleza katika namna fulani lile jambo ulilokuwa unamueleza.

Kujilinganisha
Hili nalo ni kosa kubwa ambalo linafanywa pia hata na wanaume lakini zaidi wanawake. Baadhi ya wanawake wana kasumba ya kupenda kujilinganisha maisha ya wenzao na kutaka wafanyiwe na wenzi wao. Hili ni kosa. Uhusiano wenu unapaswa kuwa wenu.

Msiwaige watu wanavyoishi, usijaribu kujilinganisha nao halafu ndio utake kufanana
nao, ishini maisha yenu, wekeni ndoto zenu mnazotaka kuzifikia. Mathalan unataka uwe na mapazia, makochi au rangi nzuri ya nyumba, mavazi na kadhalika, wekeni mikakati yenu na mjue namna ya kufikia mafanikio yenu. Msilaumiane kuyakosa mafanikio. Tengenezeni mfumo wa kuyafikia malengo yenu katika muda muafaka.

Ubize na marafiki
Hili nalo ni tatizo. Wapo baadhi ya wanawake ambao wanajisahau. Kipaumbele cha maisha yao wanakitoa kwa marafiki au familia na kumfanya mwanaume wake kama mtu wa ziada. Unapaswa kumpa thamani mwanaume wako kuliko mtu mwingine yeyote. Onesha jinsi unavyomheshimu, anapofika nyumbani hata kama ulikuwa na mazungumzo na marafiki au wageni wowote basi onesha kumjali mumeo. Siyo anafika wewe upo bize tu na marafiki au watoto wako. Muoneshe unamjali,
unamthamini na unampa kipaumbele maishani mwako. Ukifanya hivyo utamfanya mwanaume ajisikie yupo wenye mikono salama na atazidi kukupenda kwelikweli

Read More

Jinsi ya kuwa mke mwema

Mwanamke mwema hujengwa kwa misingi ya mienendo na tabia za mtu huyo. Ili ili mwanamke aweze kuwa mwema anahitaji mambo yafuatayo;

Uhalisi wa maisha
Maisha halisi ya mwanamke anayetarajia kuwa mke/ mke tayari hii ni kumaanisha kuwa wanawake mashujaa tunapaswa kuishi maisha ambayo yanatutambulisha kama mfano wa kuigwa ili tunapozungumza na kufundisha mabadiliko tuwe tunazungumza uhalisia wa maisha yetu ambao unajengwa na haya yafuatayo;

Uvumilivu
Kuwa mvumilivu katika maisha yake ya kila siku hasa ukizingatia kuwa tunakutana na mambo mbali mbali yasiyotuvutia katika mahusiano yetu, mengine ni magumu na yanayokwenda kinyume kabisa na matakwa yetu au mazoea yetu ya binafsi. Ifahamike kwamba wewe kama mwanamke shujaa inapotokea umekutana na mambo kama haya hupaswi kuonyesha hasira zako wazi wazi kama vile; chuki, kulaumu, ugomvi, vurugu, malalamiko, manung’uniko, machafuko, kulipa kisasi au aina yoyote ya uharibifu kutokea kwako au ndani mwako. Hivyo mwanamke shujaa huwa ni heri kila anapokuwa kwani hutunza amani ya eneo alipo.

Upendo wa dhati
Maisha ya upendo wa halisi na sio wa kinafki kwa jamii inayomzunguka. Tabia ya upendo wa halisi ina thamani kubwa sana kuliko mali nyingi, pesa, elimu ya juu n.k. wewe unaweza kabisa kuwa na elimu ya juu sana na pesa nyingi sana lakini pasipo upendo wa halisi ni sawa na kusema kopo zuri kwa nje na ndani hamna kitu. Nguzo kuu ya maisha ya mwanamke shujaa ni Upendo wa dhati na uhalisia.

Utii kwa kwa jamii
Maisha halisi ya utii katika jamii inayokuzunguka  ili kuweza kuyafanyia kazi yale yote uliyojifunza na pia kuyatenda kwa ufasaha pasipo kupita kona yoyote. Utii  kwa jamii ni ufunguo mmoja wapo utakaokusaidia kufanikisha mambo yako na malengo yako kama mwanamke shujaa.

Uaminifu katika jamii
Kuishi maisha ya uaminifu wa kweli na uhalisia katika jamii inayomzunguka. Uaminifu wa kweli huonekana nyakati zote na siyo tu wakati mtu anapokuwa mbele za watu wanaomjua bali hata wale wasiomjua na hata anapokuwa mahali peke yake aweze kutunza uaminifu wake kwa faida ya jamii nzima. Mwanamke shujaa hujitahidi sana kutunza uaminifu wake katika sekta zote.

Unyenyekevu wa kweli
Kuishi maisha halisi kabisa ya unyenyekevu kwa jamii inayomzunguka, unyenyekevu ni kinyume kabisa na kiburi, majivuno, kujigamba, kujikweza, kujiinua, kujiona,na hata kjitanguliza mbele kwa kila jambo. Mwanamke shujaa huwa ni mnyenyekevu wakati wote na hana makuu daima.

Uwajibikaji wa dhati
Maisha halisi ya uwajibikaji akiangalia majukumu yake yote yanayomkabili na kuhakikisha anafanya kwa moyo bila kuwa na tabia ya kusaidiwa majukumu yake. Mwanamke shujaa ni mfano wa kuigwa kutokana na uwajibikaji wake.

Ushirikiano wa dhati
Ushirikiano katika jamii inayomzunguka. Sisi wanawake mashujaa yatupasa kujua dhahiri kuwa kazi ya kubadili tabia na kufanya wengine wabadilike kwa lengo la kupata familia bora ni lazima kuwa na ushirikiano wa kweli ambao utajenga tabia ya kuaminiana na kunai mamoja katika harakati hizi za kuandaa/ kujenga familia bora.

Utaratibu wa kazi/mpangilio
Katika utaratibu wa maisha yake, pamoja na mpangilio mzuri wa mambo yanayomzunguka hii itakusaidia kuwa na muda mzuri wa kufanya shughuli zako na pia kutekeleza majukumu yako ya kila siku kama mwanamke shujaa. Hakuna njia yoyote ya kukuwezesha kukua na kuendelea katika maisha yako bila kuwa na utaratibu na mpangilio wa mambo yako.

Kufanya tathimini


Kuweza kufanya tathimini ya yale yote anayoyafanya katika maisha yake ya kila siku, pengine ni mfanyabiashara, mfanyakazi, mkulima n.k kama mwanamke shujaa yakupasa kutathimini shughuli zako kama zinaleta faida/hasara kwa familia na jamii yako inayokuzunguka. Ukiona faida ni kubwa unaendelea na hiyo shughuli lakini kama hasara ni kubwa unajiweka katika nafasi ya kubadilisha aina ya shughuli mara moja bila kupoteza wakati.
 (SOURCE, MUUNGWANA BLOG, May 23, 2020)

Read More