CHRISSHALOM NA AY





Chrisshalom muimbaji wa Gospel kutoka Nigeria amepost katika ukurasa wake wa instagram kuwa muda sio mrefu atatambulisha wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la AY . Chrisshalom ametaja majina ya nyimbo zake tatu. Power belongs to you, My beutifier , You are the reason na kusema kuwa hivi sasa tarajia Ay .
Read More

MUNGU HATAFUNGUA MILANGO TB JOSHUA


Mtumishi wa Mungu Tb Joshua kutoka Nigeria ameshare na wewe kuwa Mungu hatafungua milango ya hekima kwa yeyote anae weka Biblia chini  na kusema kuwa  anakutia  moyo kusoma neno la Mungu  taratibu na kwa makini tena mara kwa mara pia utafakari katika neno mpaka itakapo kuwa kweli kwako .

Read More

ALICHOSEMA MZEE WA PAUKO BAADA YA KUZUSHIWA KIFO




Mchungaji Anthony Lusekelo maarufu kama Mzee wa Upako kutoka kanisala maombezi (GRC) siku ya jana habari zilikuwa nyingi kuwa amefariki dunia mara yupo mahututi. Mzee wa upakao amekanusha habari hizo baada ya kupost video akiongea kuwa Yupo salama kabisa na anamshukuru Mungu anaamini ipo siku atakufa lakini sio leo.
Read More

TATIZO SIO WEMBAMBA TU NILIKUWA NA DHIKI NYINGI MARTHA MWAIPAJA ( VIDEO)


Martha Mwaipaja muimbaji wa  Gospel Tanzania ameshare na wewe mambo mengi kuhusu maisha yake katika Exclusive interview ya Chomoza tv ameelezea kipindi anatambulisha wimbo wake wa usikate tamaa Martha amesema pamoja na kwamba alikuwa mwembamba alikuwa na dhiki nyingi katika maisha yake na kwamba maisha ya Martha wa leo sio ya jana tazama video hapa chini.
Read More

PESA HAIKUFANYI KUWA MTUMISHI MKUBWA ANGEL BENARD


Angel Benard asubuhi leo ametoa somo kwa watu kuwa kuwa na pesa hakukufanyi kuwa mtumishi wa Mungu mkubwa Angel ametoa mfano kwenye biblia. Ambao unaomuonesha Petro katika Matendo ya mitume 3:6 ambapo alisema kuwa sina fedha wala dhahabu lakini nilichonacho ndicho nikupacho .


ANGELBENARDOFFICIAL

Matendo3:6
Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende.
Read More

GOODLUCK GOZBERT: NILIOMBA KWA AJILI YAKO OMMY DIMPOZ

Ommydimpoz ambae alizungumza katika kipindi cha Dadaz na kusema kuwa wakati anaumwa alikuwa akifarijiwa na nyimbo za Goodluck Gozbert . Goodluck amepost video Ommy akisema hivyo na kusema popote ulipo na unasikiliza nyimbo zake anajivunia wewe lakini pia anakuombea kutoku kata tamaa kwa hali zote.
Goodluck amesema asante Ommy dimpoz niliomba kwa ajili yako na leo nina furaha upo hapa pamoja nasi .
Read More

MPAKA UBADILI MTAZAMO JESSICA HONORE




Jessica honore amekukumbusha kuwa katika maisha kuna vifungo vingine havikuachi mpaka umebadilisha mtazamo wako .Jessica amesema ni maombi yake juu yako macho yako ya ndani yakafunguke ukatambue yaliyofichika katika ufunuo wa Kiungu.

OFFICIALJESSICAHONORE

Kuna vifungo havitakuacha paka umebadili mtazamo wako!
Ni maombi yangu macho yako ya ndani yakafunguke na ukaone vyema na ukatambue yaliyofichika katika ufunuo wa kiungu!
Ukaone raha ya uhuru aliokupa Yesu

Read More

UFALME WA MUNGU SIO WA HISIA




Mercy Masika muimbaji wa Gospel Kutoka nchini Kenya amesema watu wengi wamekuwa wakisema hawajisiki kuomba mara hawa hisi nguvu ya Mungu kuwepo Mercy amesema huu ufalme wa Mungu sio wa hisia na adui akijua wewe unatembea kwa hisia atafanya chochote kuhakikisha huombi . Atafanya chochote ujisikie uchovu usisome neno la Mungu maamuzi ambayo unatakiwa kufanya ni kuamua kusema mimi nitaomba , mimi sitawaambia watu navyojisikia bali sitaendeshwa na hisia bali na Roho Mtakatifu.
Read More

TUNA HATARI ZAIDI AMBWENE MWASONGWE








Ambwne Mwasongwe muimbaji Gospel Tanzania amesema wao wanaosimama mbele za watu wanahatari zaidi amesema watu wengi wanaimba wakidhani wanamwabudi Mungu , wanapiga vyombo kwa ustadi ,wanaruka,wanaomba .Lakini yawapasa kufahamu kuwa tendo lolote la Ibada ambalo halijampa Mungu nafasi ya kwanza haliwi ibada kwa Mungu.


Kama utasimama mbele na kuimba mtazamo wako ukawa ni kuwafurahisha watu basi umewaabudu hao watu kama utacheza step nzuri sana ili watu wakuone basi hujamwabudu Mungu. Umeabudu uliowapa nafasi.
Kama utasimama mbele na kuimba huku mtazamo wako ni kuwafurahisha watu basi umeabudu hao watu, kama utacheza step nzuri sana ili watu wakuone basi hujamwabudu Mungu umeabudu uliowapa NAFASI, kama umefunga ili watu wakuone una uwezo wa kufunga umeshapata thawabu kwa watu hao na si kwa Mungu. NDIO MAANA NI VIBAYA SANA KUTAKA MAONI YA ULIVYOIMBA, HUBIRI, CHEZA NK KWA WATU MAANA UNAKUWA UMEKWAMA KUMUABUDU ANAYESTAHILI KUPOKEA HUO UTUKUFU BADALA YAKE UMEUPOKEA WEWE.
Read More