MOJA YA KANISA LA KALE RUNGWE

 

Moja ya kanisa linalotajwa kuwa la kale zaidi wilayani Rungwe. Kanisa hili linapatikana kijiji cha Ndubi/ Kisa, Kata ya Kisondela .

Read More

MAANA YA PALLIUM





Hili ni vazi ambalo huvaliwa na Baba Mtakatifu, Maaskofu Wakuu na Patriaki wa Yerusalem tu. Ieleweke wazi kuwa siyo kila Askofu Mkuu huvaa Pallium. La hasha! Huvaliwa tu na Maaskofu Wakuu ambao ni Maaskofu-Jimbo (yaani wana majimbo wanayoyaongoza).
Hata hivyo, huvaliwa tu na Askofu Mkuu awapo ndani ya majimbo yanayounda Jimbo Kuu lake. Mfano Jimbo Kuu la Mwanza linaundwa na majimbo ya Mwanza, Musoma, Shinyanga, Bunda, Geita, Kayanga, Bukoba na Rulenge-Ngara. Hivyo Askofu Mkuu wa Mwanza anaweza kuvaa Pallium awapo kwenye mojawapo ya majimbo hayo. Akienda Jimbo la Tanga, kwa mfano, hawezi kuvaa Pallium kwa sababu ni nje ya metropolitan yake (nje ya mipaka ya Jimbo Kuu la Mwanza).
Pallium hutokana na sufu (manyoya ya kondoo) yaliyokatwa kutoka kwa kondoo wakati wa sherehe ya Mt. Anyesi ambayo huadhimishwa Januari 21 kila mwaka. Jina Anyesi (au Agnes) limetokana na neno la Kilatin “Agnus” lenye maana ya “Mwanakondoo”. Kwa nini hutengenezwa kutokana na sufu ya kondoo? Kwenye Agano Jipya Kristo anatambulishwa kama “Mwanakondoo wa Mungu” (rejea Yn. 1:29, 36). Kama ambavyo kondoo wanatoa sufu kwa ajili ya kutengeneza Pallium.
hivyo hivyo Kristo aliye “mwanakondoo wa Mungu” anajitoa sadaka kwa ajili ya dhambi za ulimwengu. Kadhalika, kitendo cha kuvaa shingoni Pallium iliyotengenezwa kutokana na sufu ya kondoo kinaonesha kuwa Askofu ni Mchungaji Mwema kwani amewabeba kondoo zake (waamini) mabegani. Pallium inapovaliwa shingoni mwa Askofu inamaanisha pia “nira ya Kristo” kwani Kristo alisema “Jitieni nira yangu… Kwa maana nira yangu ni laini…” (Mt. 11:29, 30). Pallium zikishatengenezwa huweka chini ya altare ya Basilica la Mt. Petro karibu kabisa na kaburi la Mtume Petro. Kila tarehe 29 June ambayo ni Sherehe ya Watakatifu Petro na Paulo Mitume, Maaskofu Wakuu wapya walioteuliwa mwaka huo huenda Roma na kupatiwa Pallium hizo kama zawadi maalumu kutoka kwa Baba Mtakatifu.
Kwa nini Pallium huwekwa karibu na kaburi la Mtume Petro? Na kwa nini Papa pekee ndiye huwapatia Pallium Maaskofu Wakuu? Hii ni kuonesha kuwa Maaskofu Wakuu wanapaswa kuwa na ushirika wa kipekee kabisa na Baba Mtakatifu ambaye ni halifa wa Mtume Petro. Wanapaswa kuonesha muungano na utii kwa Baba Mtakatifu ambaye ni halifa wa Mtume Petro. Pallium ni nyeupe ili kuonesha kuwa Askofu husika anapaswa kuwa na usafi wa maisha (innocence of life).
Padre Kelvin Onesmo Mkama, Jimbo Kuu la Mwanza

(ARTICLE FROM TEC FACEBOOK, 2020)
Read More

Mwelekeo Mpya wa FPCT Tanzania

 



Katika awamu ya tano  ya  Kanisa  la FPCT  chini ya  uongozi wa Askofu Mkuu , Mch Stevie Mulenga, Mungu ametupa neema ya mwelekeo au dira  inayofahamika kama  4U. Lengo  kubwa  likiwa kusimamia  katiba yetu, kurahisisha utekelezaji wa mpango mkakati wa FPCT  wa miaka 10 pamoja  na  miongozo  na sera  mbalimbali  za uendeshaji  wa  shughuli  za  kila  siku  ndani  ya kanisa FPCT. Mpango  huu  unasisitiza  na kuhamasisha  mambo  yafuatayo;

Uinjilisti  na Umisheni

Uwajibikaji  na  Uwajibishwaji,

Uchumi  na  Uchangiaji,

Uadilifu  na Uaminifu

4U kama  linavyotamkwa  katika  lugha  ya  kiingereza  linaweza  kumaanisha”For You” linamaanisha  “Ya kwako”.Yaani  mpangp  huu  ni  wa  kwako  na  hasa  kwa  mwana FPCT au mdau  yeyote wa kanisa  hili.Haya  mambo  yanayohamasishwa  na uongozi  mkuu  wa kanisa  ni  ya kwako si  ya  mtu  mwingine. kwa  hiyo  basi  tukizungumzia  Uinjilisti  na Umisheni  ni  wa  kwako  si wa mtu  mwingine,mtu  mwingine  anaweza  kuja  kuuunga  mkono  juhudi  za kwako  ambazo  zinaendelea  na hata  akiondoka  kwa sababu  ni ya  kwako  basi  wewe  unaendelea. Tunapozungumzia Uwajibikaji  na  Uwajibishwaji  nao  ni wa kwako  si  wa  mtu  mwingine   anayepaswa  kuwajibika  katika  eneo  lako  kama  kiongozi  wa  kanisa  ngazi  yoyote, kiongozi  wa  idara  au  taasisi  uwajibikaji  ni  wa kwako. Uadilifu  na Uaminifu   si  jambo  la  jumla lazima aanze  mtu  mmoja  na  kuwa  kielelezo  kwa watu  wengine. Katika  Uchumi  na Uchangiaji hii  nayo  ni  ya  kwako, mchangiaji si  mtu  kutoka  nje  ya kanisa letu, kama  atakuja  mtu  wa  nje  atakuwa  wa msimu  au  vipindi  Fulani  lakini  hii  ni  ya  kwako [For You]. Kimsingi  wote  tunakubaliana  kuwa  kitu  cha  kwako  lazima  ukijali, ukitunze, ukiboreshe, ukigharimikie, ukipende, ukipe  kipaumbele.

(ARTICLE FROM FPCT WEBSITE,2020)

Read More

Orodha ya Makanisa FPCT Tanzania

 



Takwimu zinaonyesha hadi sasa kuna;

MAJIMBO 24,
MAKANISA YA MAHALI 274,
PARISHI 1098,
MATAWI 4680 na
Kazi Mpya 686.


(ARTICLE FROM FPCT WEBSITE, 2020)
Read More

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YATANGAZA MAENEO RASMI YA KUANZISHA BUCHA ZA WANYAMAPORI



 BAADA ya watanzania kusubri kwa muda mrefu kufunguliwa kwa bucha za Wanyayapori hapa nchini hatimaye Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt.Aloyce K.Nzuki, ametangaza rasmi maeneo ya  kuanzisha bucha za Wanyamapori.

Akitoa taarifa hiyo mbele waandishi wa habari leo katika Ofisi za makao makuu ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania( TAWA) Mkoani Morogoro, Katibu Mkuu huyo ametangaza Mikoa 23 ya Tanzania Bara ambayo itaanza kufungua Bucha za wanayapori.

Amesema kuwa Mikoa iliyosalia ikiwemo Mikoa ya Songwe, Mara na Rukwa nayo itapewa fursa ya kuuza kitoweo hicho baada ya kukamilika kwa utaratibu wa kiutendaji ambao umewekwa na mamlaka hiyo.

 Sambamba na uanzishwaji wa majengo ya bucha za Wanyamapori,Wizara imeweka vigezo vya Magari maalum yatakayotumika kubeba na kuuza Nyamapori(mobile butcher) katika maeneo mbalimbali nchini.

Hata hivyo ameeleza kuwa mpaka sasa TAWA imepokea jumla ya maombi 25 ya watanzania wanaokusudia kuanzisha bucha za Wanyamapori, na  amewataka watu kujitokeza kwa wingi na kuchangamkia fursa ya kutuma maombi ndani ya siku 14 kuanzia tarehe 25.09.2020 ili kuwahi kalenda ya vikao vya kamati ya kupitisha maombi,ambayo inakutana mara nne kwa mwaka.

(Article From Issa Michuzi Blog, 2020)

Read More

NI MUNGU PEKEE NDIYE ANAYEDUMU MILELE

 






Mfanye Mungu awe kila kitu katika Maisha yako wala usizipe nafasi changamoto maana Mungu uliyenaye ni Mkubwa kuliko hizo changamoto.
Wakati mwingine changamoto zipo na ni nyingi sana na haujui hata ufanye nini, inafika mahali unakata tamaa kwa maana hauoni njia ya kutoka; Mwanangu usizitazame hizo changamoto zitatoweka, hakuna changamoto zinazodumu milele bali ni za kitambo tu, NI MUNGU PEKEE NDIYE ANAYEDUMU MILELE muangalie YEYE, mruhusu awe na wewe wakati wote na Tumaini lako uweke kwake hakika atakuvusha salama.
Zaburi 121:1-3 “Nitayainua macho yangu niitazame milima, Msaada wangu utatoka wapi? Msaada wangu u katika BWANA, Aliyezifanya mbingu na nchi. Asiuache mguu wako usogezwe; Asisinzie akulindaye;”
© MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA – KANISA LA EFATHA.
Read More

Mgombea Urais CHADEMA Anena

 


"Tunataka maamuzi ya Ardhi ya Karagwe, yafanywe na watu wa Karagwe, sio wageni tunataka mambo yanayotuhusu wananchi wa Karagwe, Singida, Dodoma au Chato, wafanye wananchi wenyewe, ndio maana ya utawala wa Majimbo tunaouzungumzia"- @TunduALissu

Read More

Mama Mzazi wa Muugizaji Maarufu RAMBO afariki dunia

 







Mama mzazi wa mcheza sinema maarufu wa Hollywood, Sylvester Stallone aka Rambo, Jackie Stallone, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 98.

Kupitia ukurasa wake wa twitter, mwanaye mdogo Frank Stallone ameandika kuwa mama yao huyo amefariki akiwa usingizini na kuongeza kuwa wamepokea kifo hicho kwa uchungu na maumivu makubwa.
“Asubuhi ya leo, kaka zangu na mimi tumempoteza mama yetu Jackie Stallone. Aliyekuwa mama wa watoto wanne, Tommy, Sylvester, Frankie na marehemu dada yetu Toni Ann.” aliandika Frank mdogo wake Sylvester.
Katika Twitter hiyo, Frank ameongeza kuwa, mama yao alikuwa mchapakazi na mwenye kupenda usawa na aliwalea vyema licha ya kuondokewa na mumewe ambaye aliwazaa yeye na kaka yake Sylvester aliyekuwa mwanasheria tajiri na kisha kuolewa tena.
Mama wa mcheza sinema huyo maarufu, alizaliwa Novemba 29, 1921 huko Washington DC na ameacha wajukuu Saba na vitukuu Watatu.
Muda wa maisha yake, kwa mujibu wa Frank, kaka yake Sylvester alikuwa akimlea mwanamke huyo kama malkia.
Read More

Makosa yanayofanywa na wanawake wengi katika mahusiano ya kimapenzi

 

Hakuna kitu kizuri kwenye uhusiano kama kuishi vizuri, uhusiano usiwe na ugomviugomvi wa kila mara. Kila mmoja aujue wajibu wake kwa mwenzake, amsome mwenzake ni mtu wa aina gani ili kuweza kujua namna ya kuishi naye. Mathalan ni vyema kumsoma mwenzi wako kama ni mtu wa hasira sana, ujue namna ya kuishi naye. Anapokuwa na hasira, usimueleze kosa lake au kumkosoa. Subiri hasira zitakaposhuka, mueleze katika lugha rafiki na hapo utakuwa umeepusha mengi.

Kumueleza mtu makosa yake katika wakati ambao naye ana hasira, utasababisha hasira zimpande zaidi na kusababisha hata ugomvi mkubwa hivyo busara zaidi zinapaswa kutumika. Mjue mwenzi wako ni mtu wa aina gani kisha ishi naye kwa staili unayoona inafaa. Kuna makosa mengi ambayo huwa wapendanao wanayafanya lakini katika makala haya leo nitazungumzia makosa ambayo ni hatari na yanafanywa na wanawake kwa wanaume wao.

Kung’ang’ania jambo
Mara nyingi wanaume huwa hawapendi kuona mwanamke anang’ang’ania jambo moja kwa muda mrefu. Hawapendi kuona mwanamke anashinikiza jambo kwa kiasi ambacho kinamnyima amani. Hata kama unajua upo sahihi, mwanamke unapaswa kutoonesha uking’ang’anizi kwa mwanaume wako. Mueleze mara moja jambo, mara ya pili ukiona hakuelewi muache kwanza.

Anakuwa anapima jambo lako na wakati mwingine akili yake inakubaliana na kile unachomueleza lakini namna unavyomng’ang’ania, unavyomshinikiza anaweza akajisikia vibaya. Mueleze mara moja, mara ya pili kisha wewe hamia kwenye mada nyingine. Utamkumbushia tena kesho au kesho kutwa na si lazima utake jambo hilo umueleze siku hiyo na siku hiyohiyo upate jibu la kueleweka. Anaweza asikuelewe siku hiyo lakini kesho yake ukaona mwenyewe ametekeleza katika namna fulani lile jambo ulilokuwa unamueleza.

Kujilinganisha
Hili nalo ni kosa kubwa ambalo linafanywa pia hata na wanaume lakini zaidi wanawake. Baadhi ya wanawake wana kasumba ya kupenda kujilinganisha maisha ya wenzao na kutaka wafanyiwe na wenzi wao. Hili ni kosa. Uhusiano wenu unapaswa kuwa wenu.

Msiwaige watu wanavyoishi, usijaribu kujilinganisha nao halafu ndio utake kufanana
nao, ishini maisha yenu, wekeni ndoto zenu mnazotaka kuzifikia. Mathalan unataka uwe na mapazia, makochi au rangi nzuri ya nyumba, mavazi na kadhalika, wekeni mikakati yenu na mjue namna ya kufikia mafanikio yenu. Msilaumiane kuyakosa mafanikio. Tengenezeni mfumo wa kuyafikia malengo yenu katika muda muafaka.

Ubize na marafiki
Hili nalo ni tatizo. Wapo baadhi ya wanawake ambao wanajisahau. Kipaumbele cha maisha yao wanakitoa kwa marafiki au familia na kumfanya mwanaume wake kama mtu wa ziada. Unapaswa kumpa thamani mwanaume wako kuliko mtu mwingine yeyote. Onesha jinsi unavyomheshimu, anapofika nyumbani hata kama ulikuwa na mazungumzo na marafiki au wageni wowote basi onesha kumjali mumeo. Siyo anafika wewe upo bize tu na marafiki au watoto wako. Muoneshe unamjali,
unamthamini na unampa kipaumbele maishani mwako. Ukifanya hivyo utamfanya mwanaume ajisikie yupo wenye mikono salama na atazidi kukupenda kwelikweli

Read More