Moja ya kanisa linalotajwa kuwa la kale zaidi wilayani Rungwe. Kanisa hili linapatikana kijiji cha Ndubi/ Kisa, Kata ya Kisondela .
christian online services- East Africa No.1 Gospel platform for Tanzania, Kenya, Rwanda, Burundi and South Sudan
Moja ya kanisa linalotajwa kuwa la kale zaidi wilayani Rungwe. Kanisa hili linapatikana kijiji cha Ndubi/ Kisa, Kata ya Kisondela .
Katika awamu ya tano ya Kanisa la FPCT chini ya uongozi wa Askofu Mkuu , Mch Stevie Mulenga, Mungu ametupa neema ya mwelekeo au dira inayofahamika kama 4U. Lengo kubwa likiwa kusimamia katiba yetu, kurahisisha utekelezaji wa mpango mkakati wa FPCT wa miaka 10 pamoja na miongozo na sera mbalimbali za uendeshaji wa shughuli za kila siku ndani ya kanisa FPCT. Mpango huu unasisitiza na kuhamasisha mambo yafuatayo;
Uinjilisti na Umisheni
Uwajibikaji na Uwajibishwaji,
Uchumi na Uchangiaji,
Uadilifu na Uaminifu
4U kama linavyotamkwa katika lugha ya kiingereza linaweza kumaanisha”For You” linamaanisha “Ya kwako”.Yaani mpangp huu ni wa kwako na hasa kwa mwana FPCT au mdau yeyote wa kanisa hili.Haya mambo yanayohamasishwa na uongozi mkuu wa kanisa ni ya kwako si ya mtu mwingine. kwa hiyo basi tukizungumzia Uinjilisti na Umisheni ni wa kwako si wa mtu mwingine,mtu mwingine anaweza kuja kuuunga mkono juhudi za kwako ambazo zinaendelea na hata akiondoka kwa sababu ni ya kwako basi wewe unaendelea. Tunapozungumzia Uwajibikaji na Uwajibishwaji nao ni wa kwako si wa mtu mwingine anayepaswa kuwajibika katika eneo lako kama kiongozi wa kanisa ngazi yoyote, kiongozi wa idara au taasisi uwajibikaji ni wa kwako. Uadilifu na Uaminifu si jambo la jumla lazima aanze mtu mmoja na kuwa kielelezo kwa watu wengine. Katika Uchumi na Uchangiaji hii nayo ni ya kwako, mchangiaji si mtu kutoka nje ya kanisa letu, kama atakuja mtu wa nje atakuwa wa msimu au vipindi Fulani lakini hii ni ya kwako [For You]. Kimsingi wote tunakubaliana kuwa kitu cha kwako lazima ukijali, ukitunze, ukiboreshe, ukigharimikie, ukipende, ukipe kipaumbele.
(ARTICLE FROM FPCT WEBSITE,2020)
BAADA ya watanzania kusubri kwa muda mrefu kufunguliwa kwa bucha za Wanyayapori hapa nchini hatimaye Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt.Aloyce K.Nzuki, ametangaza rasmi maeneo ya kuanzisha bucha za Wanyamapori.
Akitoa taarifa hiyo mbele waandishi wa habari leo katika Ofisi za makao makuu ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania( TAWA) Mkoani Morogoro, Katibu Mkuu huyo ametangaza Mikoa 23 ya Tanzania Bara ambayo itaanza kufungua Bucha za wanayapori.
Amesema kuwa Mikoa iliyosalia ikiwemo Mikoa ya Songwe, Mara na Rukwa nayo itapewa fursa ya kuuza kitoweo hicho baada ya kukamilika kwa utaratibu wa kiutendaji ambao umewekwa na mamlaka hiyo.
Sambamba na uanzishwaji wa majengo ya bucha za Wanyamapori,Wizara imeweka vigezo vya Magari maalum yatakayotumika kubeba na kuuza Nyamapori(mobile butcher) katika maeneo mbalimbali nchini.
Hata hivyo ameeleza kuwa mpaka sasa TAWA imepokea jumla ya maombi 25 ya watanzania wanaokusudia kuanzisha bucha za Wanyamapori, na amewataka watu kujitokeza kwa wingi na kuchangamkia fursa ya kutuma maombi ndani ya siku 14 kuanzia tarehe 25.09.2020 ili kuwahi kalenda ya vikao vya kamati ya kupitisha maombi,ambayo inakutana mara nne kwa mwaka.
(Article From Issa Michuzi Blog, 2020)
Mama mzazi wa mcheza sinema maarufu wa Hollywood, Sylvester Stallone aka Rambo, Jackie Stallone, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 98.
Hakuna kitu kizuri kwenye uhusiano kama kuishi vizuri, uhusiano usiwe na ugomviugomvi wa kila mara. Kila mmoja aujue wajibu wake kwa mwenzake, amsome mwenzake ni mtu wa aina gani ili kuweza kujua namna ya kuishi naye. Mathalan ni vyema kumsoma mwenzi wako kama ni mtu wa hasira sana, ujue namna ya kuishi naye. Anapokuwa na hasira, usimueleze kosa lake au kumkosoa. Subiri hasira zitakaposhuka, mueleze katika lugha rafiki na hapo utakuwa umeepusha mengi.
Kumueleza mtu makosa yake katika wakati ambao naye ana hasira, utasababisha hasira zimpande zaidi na kusababisha hata ugomvi mkubwa hivyo busara zaidi zinapaswa kutumika. Mjue mwenzi wako ni mtu wa aina gani kisha ishi naye kwa staili unayoona inafaa. Kuna makosa mengi ambayo huwa wapendanao wanayafanya lakini katika makala haya leo nitazungumzia makosa ambayo ni hatari na yanafanywa na wanawake kwa wanaume wao.
Kung’ang’ania jambo
Mara nyingi wanaume huwa hawapendi kuona mwanamke anang’ang’ania jambo moja kwa muda mrefu. Hawapendi kuona mwanamke anashinikiza jambo kwa kiasi ambacho kinamnyima amani. Hata kama unajua upo sahihi, mwanamke unapaswa kutoonesha uking’ang’anizi kwa mwanaume wako. Mueleze mara moja jambo, mara ya pili ukiona hakuelewi muache kwanza.
Anakuwa anapima jambo lako na wakati mwingine akili yake inakubaliana na kile unachomueleza lakini namna unavyomng’ang’ania, unavyomshinikiza anaweza akajisikia vibaya. Mueleze mara moja, mara ya pili kisha wewe hamia kwenye mada nyingine. Utamkumbushia tena kesho au kesho kutwa na si lazima utake jambo hilo umueleze siku hiyo na siku hiyohiyo upate jibu la kueleweka. Anaweza asikuelewe siku hiyo lakini kesho yake ukaona mwenyewe ametekeleza katika namna fulani lile jambo ulilokuwa unamueleza.
Kujilinganisha
Hili nalo ni kosa kubwa ambalo linafanywa pia hata na wanaume lakini zaidi wanawake. Baadhi ya wanawake wana kasumba ya kupenda kujilinganisha maisha ya wenzao na kutaka wafanyiwe na wenzi wao. Hili ni kosa. Uhusiano wenu unapaswa kuwa wenu.
Msiwaige watu wanavyoishi, usijaribu kujilinganisha nao halafu ndio utake kufanana
nao, ishini maisha yenu, wekeni ndoto zenu mnazotaka kuzifikia. Mathalan unataka uwe na mapazia, makochi au rangi nzuri ya nyumba, mavazi na kadhalika, wekeni mikakati yenu na mjue namna ya kufikia mafanikio yenu. Msilaumiane kuyakosa mafanikio. Tengenezeni mfumo wa kuyafikia malengo yenu katika muda muafaka.
Ubize na marafiki
Hili nalo ni tatizo. Wapo baadhi ya wanawake ambao wanajisahau. Kipaumbele cha maisha yao wanakitoa kwa marafiki au familia na kumfanya mwanaume wake kama mtu wa ziada. Unapaswa kumpa thamani mwanaume wako kuliko mtu mwingine yeyote. Onesha jinsi unavyomheshimu, anapofika nyumbani hata kama ulikuwa na mazungumzo na marafiki au wageni wowote basi onesha kumjali mumeo. Siyo anafika wewe upo bize tu na marafiki au watoto wako. Muoneshe unamjali,
unamthamini na unampa kipaumbele maishani mwako. Ukifanya hivyo utamfanya mwanaume ajisikie yupo wenye mikono salama na atazidi kukupenda kwelikweli