Showing posts with label Muhubiri. Show all posts
Showing posts with label Muhubiri. Show all posts

Balaa, Laana na mikosi ya kifamilia.

 



Mara nyingi unapoenda hospitali, daktari huwa anauliza kama kuna mtu katika ukoo wako, ana historia ya tatizo hilo na jibu lako humsaidia kujua tatizo lako kwa undani. Vivyo hivyo laana, mikosi na balaa vinaweza kufuata familia yako kama zilivyo baraka pia.

Ndio maana watoto wengi wa viongozi serikali huishia kuwa viongozi, na watoto wengi wa maskini hujikuta wanaishia kuwa katika umaskini zaidi, ni ukweli ulio dhahiri kuwa kilichotendwa na baba huwa kinashuka hadi kwa watoto wake. Ukisoma katika Mithali 13: 22 “Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi; Na mali ya mkosaji huwa akiba kwa mwenye haki.” Pia, Zaburi 37:25 “Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee, Lakini sijamwona mwenye haki ameachwa Wala mzao wake akiomba chakula.”

Adamu na Hawa walipotenda dhambi, hukumu kwa mwanamke ilikuwa hivi, Mwanzo 3:15, Mungu aliweka uadui kati ya uzao wa mwanamke na uzao wa nyoka. Kwanini unafikiri Mungu aliweka uadui hata kwa watu ambao hawakuhusika? Jibu ni kuwa yaliyotendwa na wazazi au mababu wa ukoo yana matokeo sana katika maisha ya mtu ya leo. 2Timotheo 1:3-5 “…5 nikiikumbuka imani uliyo nayo isiyo na unafiki, ambayo ilikaa kwanza katika bibi yako Loisi, na katika mama yako Eunike, nami nasadiki wewe nawe unayo.” Kumbe kuna uwezekano wa tabia ya mtu kuunganishwa na familia au ukoo wake. Kama imani yaweza kusafiri kiukoo, vivyo hivyo na tabia ya kutokuamini au uovu mwingine waweza kusafiri kutoka kwa mtu kizazi kimoja hadi kingine.

Ndio maana inawezekana, mtu akajikuta anafanya tabia fulani, na ingawa haipendi lakini anaendelea kuifanya kumbe ni kwasababu ya ukoo wake. 1Petro 1:18-19 Waweza kuumkuta mtu mwongo, mwizi, mzinzi, mchoyo, mbisho kumbe ni kwasababu ya tabia za kurithi ambazo zinatokana na laana za familia. Kuna uwezekano mtu akajikuta hana ndoa ya kudumu, kumbe ni kutokana na laana iliyo katika ukoo.

Ni muhimu kumjua adui unayepambana naye, watu wengi sana wanajikuta wanapambana na adui wasiyemjua huku wakidhani wako sahihi, na mwisho hujikuta wana bidii yao haizai matunda, kumbe ni matokeo ya kupambana na adui usiyemjua. Huwezi kushindana na shetani bilankujua mbinu zake “watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa.”

Jambo lingine la Muhimu, maamuzi yoyote unayoyafanya leo yana matokeo katika maisha yako na ya uzao wako. Ndio maana wana wa Israeli walipokuwa wanaingia katika nchi ya ahadi Yoshua aliwaambia, “chagueni hivi leo mtakaye mtumikia” uchaguzi unaoufanya leo una matokeo mazuri au mabaya katika maisha yako.

Biblia inasema kila andiko lenye pumzi ya Bwana lafaa kwa mafundisho, kwasababu hiyo tunaweza kujifunza kitu kutoka katika maisha ya baba wa Imani, Ibrahimu. Mwanzo (11:29-30), ibrahimu alikuwa hazai maana Sara alikuwa tasa, tunaona pia mwanaye Isaka naye akawa na tatizo hilohilo la kukosa mtoto kwa mkewe Rebeka (mwanzo 25:21); na jambo hilo halikuishia hapo kwani na Yakobo alipatwa na tatizo hilohilo.

Pia, kwa namna hiyihiyo ukifanya yaliyo mema mbele za Mungu, baraka zako hufuatana na uzao wako. Tunaona jambo hilo kuwa, baraka za Ibarahimu ziliweza kufuatana na uzao wake (Mwanzo 30:1-6; 13:15; 17:7-10) ahadi za Ibrahimu hazikuishia kwake tu bali zilipitiliza hadi kwa uzao wake. Kumbe baraka zaweza kusafiri kutoka kwa mababu hadi wabibi, vivyohivyo laana zaweza kusafiri kutoka kwa kizazi kimoja hadi kizazi kingine. Ndio maana hata Yoabu alipomuua Abneri, ambaye alikuwa awali amesamehewa na Mfalme Daudi, ile laana ilifika hadi kwa uzao wake.

Utajifunza pia kwa habari ya Yesu, walipotaka kumuua, wayahudi walitamka wazi kuwa “25 Watu wote wakajibu wakasema, Damu yake na iwe juu yetu, na juu ya watoto wetu.” Mathayo 27:24-26 wayahudi walijua ukweli huu kuwa laana zaweza pita kutoka uzao mboja wa uovu hadi mwingine, kwasababu hiyo inawezekana unaishi katika mateso leo kwasababu ya mambo yaliyopita huko nyuma.

Mungu hapendi kuwatesa wanadamu wala kuwahuzunisha (Maombolezo 3:33). Lazima usimame kinyume na kila laana katika familia yako na katika maisha yako, jitenge na kila laana za kutoka kwa familia au ukoo wako. Balaa, laana na mikosi ya familia yako na ivunjike katika jina la Yesu Kristo.

Na Mchungaji Josephat Gwajima



Read More

Sababu za wakristo kuabudu Jumapili

 




Siku ya JUMAPILI, ambayo ndiyo siku ya kwanza ya juma, SIKU YA BWANA aliyoshinda mauti na kufufuka [UFUNUO1:10] Tunaitenga maalum kumwabudu Bwana kwa sababu:-

a) Ni sikukuu ya malimbuko ya mavuno ambayo ilifanywa katika Agano la Kale, SIKU YA PILI baada ya Sabato; Ikiwa ni utabiri wa Kristo ambao ni LIMBUKO lao waliolala [WALAWI23:9-14;1WAKORINTHO15:20].

b) Ni siku ya ushindi ya Bwana wetu Yesu aliyofufuka, na kujidhihirisha kwa wanafunzi wake baada ya kufufuka kwa Yesu [YOHANA 20:1,19,26 WARUMI 10:9].

c) Siku ya kuja Roho Mtakatifu, Mwangalizi mkuu wa kazi yote ya Mungu katika kanisa, ilikuwa siku ya Pentekoste ambayo ni Jumapili, siku ya pili baada ya sabato [MATENDO 2:1]

d) Siku ya Pentekoste, Jumapili ndiyo siku ya kwanza ambayo kanisa la kwanza lilianza mahubiri na watu 3,000 wakaokoka na kuanza kusanyiko la kwanza la Ibada kanisani [MATENDO 2].

e) Wakristo wa kanisa la kwanza walikusanyika Jumapili [MATENDO 20:6-12;1WAKORINTHO 16:1-2].

Sababu hizi, zinadhihirisha pia wazi wazi kwamba kuabudu Jumapili hakukuanzishwa na mfalme CONSTANTINE wala kanisa Katoliki.

Hakuna andiko lolote linalosema mtu yeyote anayeabudu Jumapili ana alama ya 666 ya mnyama. Huo ni uzushi. Biblia inatupa uhuru wote katika kuchagua siku ya kumwadhimisha Bwana [WARUMI14:5-6]. Vilevile ni muhimu kufahamu kuwa siku zote ni siku za kujifunza Neno [MATENDO 17:11;2:46].

KUSHIKA SIKU, SIYO NJIA YA KUOKOKA

Kushika siku yoyote hata iwe Jumapili, sio njia ya kuokoka.Tunaokolewa kwa kumuamini Yesu kuwa ni BWANA na MWOKOZI na sio kwa kushika siku yoyote [WARUMI 10:9-10,13].

—Anin Gift

Read More

Ndoa ni nini?

 




Ndoa ni muungano kati ya mwanamke na mwanamume kuishi pamoja kama mume na mke muda wote wa maisha yao. (Sheria ya ndoa – mwaka 1971 kifungu cha 9).

i) Wanaooana wawe wamekubaliana pasipo kulazimishwa na mtu.

ii) Ndoa ni ya mwanamke na mwanamume.

iii) Ni ndoa ya kudumu maishani.

Mpango na utaratibu wa MUNGU kwa wanandoa umewekwa wazi katika kitabu cha Mwanzo.

“Bwana MUNGU akasema si vema mtu huyu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufafana naye”. Mwanzo 2:18.

Hapa tunaona kuna suala la mamlaka katika ndoa, kwamba mke ni msaidizi.

“Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja”. Mwanzo 2:24.

Hapa tunaona kusudi la MUNGU katika suala la kuachana na kuambatana. Wanandoa wanatakiwa kuachana na wazazi wao katika maeneo matatu.

i) Kimwili – wawe na makazi yao wenyewe

ii) Kihisia – wategemeane na kutiana moyo na kusaidiana

iii) Kiuchumi – wajitegemee kwa mahitaji yao ya kila siku.


TENDO LA NDOA

Ukizingatia kanuni za MUNGU kibiblia kuhusu tendo la ndoa kwa wanandoa;-

i) Ni tukio dogo lenye umuhimu mkubwa.

ii) Kusudi kubwa la tendo la ndoa ni uzazi.

iii) Ni kinga dhidi ya majaribu.

iv) Ni burudani/starehe.

v) Ni suala la kuwa na uvumilivvu na kujitoa.

NDOA -TAASISI TAKATIFU

Ndoa yenye furaha na kuheshimika ni ile ambayo kila mmoja anafahamu na kutimiza wajibu wake katika ndoa kwa mujibu wa nafasi yake. Na hii ndio sharti la msingi kutupelekea kwenye ndoa yenye mafanikio.

i) Kumheshimu mwenzi wako kutokana na hadhi aliyonayo kama MUNGU alivyoagiza.

ii) Heshima inasaidia kutuepusha na ubinafsi na kuongozwa na hisia.

iii) Heshima katika ndoa inachochea mapenzi.


NDOA NI KUTOA

1. Ndio sio mkataba wa kijamii bali agano la kiroho. Waefeso 5:31-33 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. Siri hiyo ni kubwa, ila mimi nanena habari ya KRISTO  na Kanisa. Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe, wala mke asikose kumstahi mumewe.

Hapa tunajifunza

i) Ndoa ni fumbo la ajabu la kiroho linalowaunganisha watu wawili, mwanamume na mwanamke (mst.31)

ii) Ndoa ya kikristo inaliganishwa na uhusiano uliopo kati ya KRISTO na Kanisa (mst.32)

iii) Mpango wa MUNGU katika ndoa unahitaji upendo wa kujitoa sadaka kama KRISTO anavyofanya kwa Kanisa (mst.33)

2. Ndoa ya Kikristo ni kujitoa sio kupokea. Wafilipi 2:3-4 Msitende neno lolote kwa kushindana wala kwa majivuno, bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenzie kuwa bora kuliko nafsi yake mwenyewe. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.


Hapa tunajifunza

i) Kutokuwa wabinafsi

ii) Unyenyekevu

iii) Roho ya kutoa na kujitoa.

Wewe mume/mke, mahusiano yako na mwenzi wako yakoje? Unampenda mwenzi wako kama KRISTO anavyolipenda Kanisa lake?  Kama wewe ni mmojawapo wa wasiofuata kielelezo cha KRISTO katika ndoa usijisikie vibaya kwani hakuna aliye mkamilifu. Hata hivyo wajibu huu haukwepeki kwani ni agizo la MUNGU na lazima kutii maagizo yake, kumpenda MUNGU kwa moyo waklo wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote na kwa nguvu zako zote. Na kumpenda jirani yako kama nafsi yao. Marko 12:30-31. Hivyo, hii ni nafasi yako ya kumwonyesha mwenzi wako upendo ambao wa muda mrefu ameukosa, upendo ambao KRISTO ameuonyesa kwa kanisa lake.


Barikiwa sana.


— Jane Lawi Sijaona


Kwa ushauri kuhusu Mahusiano na Ndoa, wasiliana na Askofu John Bigirimana kwa Email: rnominfo57@yahoo.com


( The Information is from Structly Gospel)

Read More