Mama Samia Suluhu Hassan Kuwa Mrithi wa Rais John Pombe Magufuri

 

 
 

Mama Samia Suluhu Hassan ambaye amekuwa Makamu wa Rais toka mwaka 2015 sasa atakuwa mrithi wa rais John Magufuli ambaye amefariki jana Jumatano Machi 17.
Samia atashikilia wadhifa huo kwa kipindi kilichosalia cha cha muhula wa urais mpaka 2025, kwa mujibu wa katiba ya Tanzania.
 
Anatarajiwa kuweka rekodi ya kuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo wa juu zaidi nchini Tanzania. Pia atakuwa rais wa pili wa Tanzania kutokea Zanzibar, wa kwanza akiwa Mzee Ali Hassan Mwinyi aliyeliongoza taifa hilo kwa miaka 10 kutoka mwaka 1985 mpaka 1995.
 

No comments:

Post a Comment