Anna Tusajigwe Mwakasege, Ni Rubani aliyeuaminiwa kuendesha ndege iliyobeba mwili wa Rais Hayati Dkt John Pombe Joseph Magufuri

 


Huyu ni mmoja wa marubani wawili waliorusha ndege iliyobeba mwili wa Rais Magufuli. Anaitwa Anna Tusajigwe Mwakasege. Ni binti wa pili wa Mwalimu Christopher na mama Diana Mwakasege.
Anna alipata maono ya kuwa rubani akiwa darasa la 3 tu. Baba yake akampeleka uwanja wa ndege angalau kuona ndege "live" badala tu ya kuziona angani tu. Alipofika darasa la 5 baba yake alitembeza uwanja mdogo wa ndege Arusha ambapo alipata nafasi ya kuongea na marubani kuhusu ndoto yake, nao wakampa ushauri masomo ya kusoma ili aweze kuifikia ndoto hiyo.
Alijifunza urubani Afrika kusini, na siku anarusha ndege kwa mara ya kwanza baba yake hakulala usiku huo (hii ni story ya wakati mwingine).
Lakini kwa sasa Anna ni miongoni mwa marubani wa shirika la ndege ATCL. Kabla ya kujiunga na ATCL alifanya kazi mashirika mengine makubwa ya ndwge kama SAA na kupata uzoefu wa kuendesha ndege kubwa kama Boeing 747, Boeing 777 na Airbus A340.
Hongera
Anna kwa kuaminiwa kuendesha ndege iliyobeba mwili wa Rais. Umeweka alama kubwa kwa taifa hili, ambayo haitafutika kirahisi. Mara zote tutakapokumbuka kifo cha JPM tutakumbuka kuwa wewe kama Senior First officer na rubani mwenzio (kiongozi) ndio mlipata neema ya kubeba mwili wake.
Najua si kazi rahisi kuendesha ndege ukiwa na majonzi ya kumpoteza Rais wako lakini umeaminiwa na umeweza. Tunawaombea kwa safari ya Zanzibar, Mwanza na Chato. Wewe pamoja na cabin crew yote. Hakika wanawake mnaweza. Unaweza kumfollow kule Instagram kwa kuandika @tusajigwe01 @tusajigwe01 #TheFutureIsFemale #WomenEmpowerment #WanawakeWanaweza
 
SOURCE FROM FACEBOOK - ACCOUNT 
Malisa GJ


No comments:

Post a Comment