Waziri Ummy Mwalimu: Serikali imefanikiwa kudhibiti corona

Share it Please







Serikali imesema kuwa imefanikiwa kudhibiti na kupunguza kwa kiasi kikubwa maambukizi ya virusi vya corona huku ikiwataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari ili kuutokomeza kabisa.

Hayo yalisemwa leo na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati wa ziara yake ya kushtukiza kwenye kwenye Kituo cha Afya cha Ngamiani Jijini Tanga ambapo aliweza kuzungumza pia na wahudumu wa Afya na kupokea msaada wa vifaa vya kunawia maji kudhibiti Ugonjwa wa Covid 19 vilivyotolewa na Shirika la Water Mission Tanzania.

(MUUNGWANA BLOG, june 2020)