ANGALIZO


WEBSITE HII IPO KWA AJIRI YA WAKRISTO WOTE. HAIFUNGAMANI NA DINI AU KANISA LOLOTE LILE.

Contact Us

Christian Online Services Organization
P.O.Box 212
Bagamoyo - Pwani
Tanzania

Email: christianonlinetz@gmail.com



POWERED BY:
TCDI

Contact Us

Name

Email *

Message *

Web Traffic


CONTACT US TO BE LISTED ON CHIRISTIAN MAGAZINE

CONTACT US TO BE LISTED ON  CHIRISTIAN MAGAZINE

Search

Christian Online Membership

Follow us on Facebook

Lissu Atangaza Nia ya Kuwania Urais 2020





Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Tundu Lissu leo amezungumza kwa Mubashara kupitia ukurasa wake wa Facebook akiwa ughaibuni na kutangaza nia ya kugombea Urais nchini Tanzania katika Uchaguzi Mkuu wa October 2020.

Lissu amechukua hatua hiyo siku kadhaa tangu John Mnyika, Katibu Mkuu wa Chadema, kuwataka wanachama wenye nia ya kugombea urais wa Tanzania kupitia chama hicho, kuwasilisha taarifa zao katika ofisi yake, kuanzia tarehe 3 hadi 15 Juni 2020.

Lissu amesema, endapo atafanikiwa kuwa Rais, ataboresha uchumi wa nchi, mahusiano na jumuiya za kimataifa na nchi marafiki, utawala bora, misingi ya haki za binadamu, demokrasia na mfumo wa vyama vingi.

Amesema uchaguzi wa mwaka huu, utaamua kama Chama cha Mapinduzi (CCM), kitapata fursa ya miaka mitano mingine ya kuendelea kuharibu uchumi wa nchi na kufukarisha wananchi, au mwanzo mpya kwa Tanzania, kujiimarisha kiuchumi.

Lissu amesema, akifanikiwa kuwa Rais wa Tanzania, atahakikisha mihimili ya nchi, ikiwemo Bunge na Mahakama, inakuwa huru na kujitegemea kwenye maamuzi yake.

Amesema katika uongozi wake kama atafanikiwa kuwa Rais wa Tanzania, atavitumia vyombo vya ulinzi na usalama kulinda haki za binadamu, na si katika kukandamiza wapinzani wake, vyombo vya habari na asasi za kiraia.

Amesisitiza kuwa endapo atafanikiwa kuwa Rais, Serikali yake itaendeshwa kwa kufuata misingi ya utawala bora na sheria, inayoendana na Katiba ya nchi pamoja na mikataba ya kimataifa, ambayo Tanzania iliikubali.

Lissu amesema, akifanikiwa kuwa Rais wa Tanzania, ataponya majeraha ya wananchi pamoja na kurejesha umoja wa kitaifa, huku akisisitiza kwamba hatalipa kisasi kwa maadui zake.


(GLOBAL PUBLISHER JUNE 8 2020)

Share this:

 
Copyright © Christian Online Services - East Africa. Designed by OddThemes