ANGALIZO


WEBSITE HII IPO KWA AJIRI YA WAKRISTO WOTE. HAIFUNGAMANI NA DINI AU KANISA LOLOTE LILE.

Contact Us

Christian Online Services Organization
P.O.Box 212
Bagamoyo - Pwani
Tanzania

Email: christianonlinetz@gmail.com



POWERED BY:
TCDI

Contact Us

Name

Email *

Message *

Web Traffic


CONTACT US TO BE LISTED ON CHIRISTIAN MAGAZINE

CONTACT US TO BE LISTED ON  CHIRISTIAN MAGAZINE

Search

Christian Online Membership

Follow us on Facebook

Ujerumani yasubiri taarifa rasmi ya Marekani






Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani, Annegret Kramp-Karrenbauer amesema Ujerumani haijapokea taarifa rasmi kutoka Marekani kuhusu mpango wa nchi hiyo kuwaondoa baadhi ya wanajeshi wake Ujerumani.

Akizungumza leo na waandishi habari, Kramp-Karrenbauer amesema hawezi kuzungumzia taarifa za kwenye vyombo vya habari bila ya kuwepo uthibitisho.

Kiongozi huyo wa chama cha Christian Democratic Union, CDU amesema ukweli ni kwamba uwepo wa majeshi ya Marekani nchini Ujerumani unatumika kuimarisha usalama wa Jumuia ya Kujihami ya NATO na washirika wengine wa NATO pamoja na Marekani yenyewe.

Amesema huo ndiyo msingi ambao unaleta ushirikiano wa pamoja kati ya nchi hizo. Naye msemaji wa serikali ya Ujerumani, Steffen Seibert amesema Ujerumani itatoa tamko mara itakapopewa taarifa na Marekani.

Siku ya Ijumaa, afisa wa ngazi ya juu wa Marekani, alisema kuwa Rais Donald Trump aliliamuru jeshi la Marekani kuwaondoa askari wake 9,500 kutoka Ujerumani.

(MUUNGWANA BLOG, June 2020)

Share this:

 
Copyright © Christian Online Services - East Africa. Designed by OddThemes