Historia ya KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani Tanzania

  

 


 

Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP) ni moja ya dayosisi ishirini za Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT). Dayosisi hiyo ilianzishwa na kusajiliwa mnamo 13 Desemba 1962 na wakati huo ulijulikana kama Sinodi ya Uzaramo-Uluguru. Mnamo Desemba 1970 jina lilibadilishwa kuwa KKKT Synod ya Mashariki na Pwani hadi Desemba 1986 wakati ikabadilishwa kuwa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani.
Shughuli za misioni katika maeneo ya pwani zilianza mnamo Agosti 1887 wakati mmisionari Johann Jacob Greiner kutoka misioni ya Berlin alifika Dar es Salaam.
Dayosisi hiyo imepokea wito wake kutoka kwa Mungu mwenyewe, miongozi mingine ni kanuni za KKKT, katiba ya dayosisi pamoja na katiba na sheria za nchi. Kwa kutimiza katiba na sheria za nchi KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani imesajiliwa kisheria kama shirika la kidini nchini Tanzania na kupewa cheti cha usajili No.10525 ya 25/8000.
Eneo la kazi yetui ni Mkoa wa Dar es Salaam, Mkoa wa Pwani na visiwa vya Unguja, Pemba na Mafia. Jiografia hii imetuweka katika jiji kubwa la Dar es Salaam ambayo ni kivutio kikubwa kwa watu kutoka sehemu mbali mbali za Dunia.
Jiji ni kitovu cha kiuchumi cha nchi likiwa na nafasi nyingi kwa dayosisi na nchi yetu.
KKKT-DMP inashirikiana na inafanya kazi kwa karibu na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na shirika zisizo za serikali za ndani ya nchi. Pia inafanya kazi kwa kushirikiana au kwa uhusiano wa karibu na mashirika ya kimataifa na ya nchi kwenye bara za Afrika, Asia, Ulaya na Amerika.

No comments:

Post a Comment